logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Rais Ruto awaagiza maafisa wa serikali na wafanyikazi wa umma kutoshiriki harambee

"Hakuna afisa wa serikali au mtumishi wa umma atakayeshiriki katika michango au harambee za umma kuendelea," rais William Ruto

image
na SAMUEL MAINA

Habari05 July 2024 - 11:08

Muhtasari


  • •Alimwelekeza mwanasheria mkuu wa serikali kutengeneza njia mbadala ya michango ya hisani kwa umma.

Rais William Ruto amepiga marufuku maafisa wote wa serikali na wafanyikazi wa umma kushiriki kwenye michango ya umma na harambee.

Rais alitoa agizo hilo katika hotuba yake ya Ijumaa alasiri katika ikulu ya Nairobi.

Alimwelekeza mwanasheria mkuu wa serikali kutengeneza njia mbadala ya michango ya hisani kwa umma.

"Hakuna afisa wa serikali au mtumishi wa umma atakayeshiriki katika michango au harambee za umma kuendelea," rais William Ruto aliagiza.

Aliongeza, "Mwanasheria mkuu anaagizwa kutayarisha na kuwasilisha usajili kwa njia hii na kuwasilisha sheria  na kuwasilisha utaratibu ulioandaliwa wa michango iliyopangwa ya uwazi kwa madhumuni ya umma, hisani na uhisani."


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved