Rais Ruto afichua sababu ya kumteua tena Kindiki katika wizara ya usalama

Ruto aliyasema hayo alipokuwa akiwahutubia wakazi wa Tharaka Nithi.

Muhtasari
  • Kindiki ni miongoni mwa Mawaziri wachache waliodumisha majukumu yao katika baraza la mawaziri lililopendekezwa.
Rais William Ruto
Image: MAKTABA

Rais William Ruto ameeleza ni kwa nini alimteua Kithure Kindiki kama Waziri wa Masuala ya Ndani wiki moja baada ya kupeleka mawaziri wake wote.

Kindiki ni miongoni mwa Mawaziri wachache waliodumisha majukumu yao katika baraza la mawaziri lililopendekezwa.

Akiongea Alhamisi katika Kaunti ya Tharaka Nithi, Ruto alisema Kindiki alifanya vyema katika kulinda nchi katika Wizara ya Mambo ya Ndani na ndio maana anasalia kwenye kizimbani.

"Nawashukuru tena mmenipatia profesa Kithure Kindiki. Huyu Profesa ndio waziri wetu wa Usalama na huyu jamaa amefanya kazi nzuri. Magaidi wamekwama, Kule Lamu amepanga, kule North Rift hata majambazi wamehama," Rais alisema.

Ruto aliyasema hayo alipokuwa akiwahutubia wakazi wa Tharaka Nithi.

Ameratibiwa kwa shughuli kadhaa katika kaunti hiyo zikiwemo kuagiza miradi ya maendeleo ya maji, umeme na masoko katika kaunti hiyo.

Rais Ruto aliendelea kuwauliza wenyeji wa Tharaka Nithi iwapo Kindiki anafaa kuendelea na kazi nzuri aliyoifanya katika wizara hiyo, ambapo walimjibu kwa sauti kubwa Ndiyo.

"Huyu jamaa anatosha ama hatoshi? Aendelee ama asiendelee? hebu nione kwa mikono."

Ruto alisisitiza kuwa Kindiki anafaa kuendeleza kazi nzuri ya kuifanya nchi kuwa salama.

Ziara yake katika kaunti hiyo ilijiri siku chache baada ya Rais kuunda upya baraza lake la mawaziri kwa kumteua miongoni mwa wengine Kindiki, baada ya kuvunja baraza lake la mawaziri.

Kufikia sasa, Ruto amefanya uteuzi wa mawaziri 20.