logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Familia ya Kifalme ya Uholanzi yatangaza kuzuru Kenya

Katika hotuba iliyoandikwa na Royal House of the Netherlands ilisema kuwa ziara hiyo itaboresha uhusiano kati ya Kenya na Uholanzi

image
na OTIENO TONNY

Yanayojiri08 January 2025 - 15:46

Muhtasari


  • Majadiliano kuhusu uchumi inayoangazia kilimo endelevu  na maji zitafanyika sambamba na ziara hiyo ya Mfalme na Malkia wa Uholanzi.
  • Ziara hii inajiri miaka miwili baada ya mfalme wa Uingereza Charles wa tatu na Malkia  Camilla kufanya ziara sawa  na hiyo nchini Kenya. 


Mfalme Willem-Alexander na Malkia Máxima watafanya ziara ya kitaifa nchini Kenya, kwa mwaliko wa Rais William Ruto. Ziara hiyo itafanyika kuanzia Jumanne tarehe 18 hadi Alhamisi tarehe 20 Machi 2025.

Katika taarifa iliyoandikwa na Royal house of the Netherlands ilisema kuwa ziara hiyo itaboresha uhusiano kati ya Kenya na Uholanzi na kuonyesha ushirikiano thabiti.

‘’Ziara hii ya kwanza ya kitaifa nchini Kenya ni uthibitisho wa uhusiano mzuri na ushirikiano thabiti kati ya nchi zetu mbili. Uholanzi inataka kushiriki katika ushirikiano mpya katika maeneo mbalimbali, na kuimarisha uhusiano uliopo wa nchi,’’ Hi ni kwa mujibu wa Royal House of Netherlands.

Katika ujumbe huo waliongezea kuwa Kenya inazidi kuwa na ushawishi mkubwa katika nyanja ya kimataifa huku Uholanzi na Kenya zikidumisha uhusiano wa karibu wa kiuchumi, na zote mbili ni vitovu na lango kuu kwa maeneo makubwa.

Ujumbe huo vile vile umeonyesha jinsi Uholanzi na Kenya zinaletwa pamoja na mashirika  za kimataifa kama vile shirika la muungano la umoja la  kitaifa maarufu kwa kimombo kama United Nations UN.

‘’Ndani ya umoja wa mataifa na mashirika mengine ya kimataifa, pia, nchi zetu mbili zinafanya kazi pamoja kikamilifu kufikia malengo yanayohusiana na demokrasia, utawala wa sheria na uhuru wa mahakama. Uholanzi na Kenya pia hufanya kazi pamoja katika changamoto zinazohusiana na amani na usalama, mabadiliko ya tabia nchi na usalama wa chakula,’’ Walisema haya katika  ujumbe huo.

Majadiliano kuhusu uchumi inayoangazia kilimo endelevu  na maji yatafanyika wakati wa ziara hiyo ya mfalme na malkia wa Uholanzi.

Ziara hii inakuja miaka miwili baada ya mfalme wa Uingereza Charles wa tatu na Malkia  Camilla kufanya ziara sawa  na hiyo nchini Kenya chini ya uongozi wa rais William Ruto. Wawili hao walitembelea Kenya kutoka tarehe 31 Octoba mapaka tarehe 3 Novemba  2023.


 



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved