logo

NOW ON AIR

Listen in Live

John Dramani Mahama aliapishwa na kuingia afisini kama rais rasmi wa Ghana

Rais John Dramani Mahama ameingia rasmi madarakani kama kiongozi wa Ghana, akiashiria kurudi kwake katika urais baada ya kuhudumu kati ya 2012 - 2017

image
na OTIENO TONNY

Yanayojiri08 January 2025 - 09:16

Muhtasari


  • Katika hotuba yake ya kuapishwa, Rais John Dramani Mahama alielezea maono yake ya ufufuaji wa uchumi wa Ghana, ushirikishwaji na mageuzi ya utawala.
  • Alisisitiza uwajibikaji, uvumbuzi, na umoja, akitoa wito kwa Waghana kuungana naye katika uwekaji upya wa kitaifa ili kujenga nchi yenye ustawi na uthabiti zaidi.

John Dramani Mahama aliapishwa Jumatano 7 Januari 2025 kama rais wa Ghana baada ya kushinda uchaguzi iliofanywa tarehe 7 Desemba 2024. Sherehe hiyo ilifanyika katika uga wa Accra’s Iconic Black Star Square.

Katika uchaguzi huo chama chake John Mahama cha National Democratic Congress {NDC} ilipata ushindi wa asilimia 56.55% za kura huku chama cha      New Partriotic Party wakipata asilimia 41.61%. uchaguzi huo ulikuwa wa kihistoria kwani ni mara ya kwanza nchi ya Ghana ilipata naibu rais wa kike tangia enzi ya uhuru.. Naana Jane Opoku –Agyemang atakumbukwa kama naibu rais wa kwanza  kike wa Ghana.

Mahama alichaguliwa katika uchaguzi wa Desemba 2012 kuhudumu kama rais na kuhudumu mpaka mwaka wa 2016, ambapo aligombea kuchaguliwa tena kwa muhula wa pili katika uchaguzi wa 2016, lakini akashindwa na mgombeaji wa New Patriotic Party Nana Akufo-Addo. Hii ilimfanya kuwa rais wa kwanza katika historia ya Ghana kutoshinda muhula wa pili mfululizo.

Baadaye Mahama alikuwa tena mgombea wa urais wa chama cha NDC katika uchaguzi wa mwaka wa 2020, ambapo alishindwa na Akufo-Addo kwa mara ya pili.

Aidha, hafla hiyo ya uapisho wake  iliwaleta pamoja wageni wengi kutoka Ghana wakiwemo  makamu wawili wa rais, spika mmoja wa bunge, marais wawili wa zamani, na wakuu kadhaa wa mashirika ya kimataifa, wakiwemo wawakilishi kutoka jumuiya ya madola na benki ya maendeleo ya Afrika (AfDB).

Rais wa Nigeria Bola Ahmed Tinubu, Rais wa Kenya William Ruto ni miongoni mwa viongozi 21 wa nchi mbalimbali waliofika kushuhudia hafla hiyo ya kihistoria katika nchi ya Ghana pamoja na wajumbe kutoka umoja wa ulaya, Marekani na Uingereza.

Katika hotuba yake ya kuapishwa, Rais John Dramani Mahama alielezea maono yake ya ufufuaji wa uchumi wa Ghana, ushirikishwaji, na mageuzi ya utawala. Aliwahakikishia wafanyabiashara na wawekezaji kwamba Ghana iko wazi kwa biashara tena, akiahidi mfumo wa kodi ulio wazi na wa haki ili kuchochea ukuaji.

‘’Tutarekebisha mifumo yetu ya ushuru ili kuifanya iwe ya haki na uwazi. Jumuiya ya wafanyabiashara lazima ijue kwamba Ghana imerejea katika biashara, tunahitaji kuweka upya imani  katika nchi yetu, katika taasisi zetu na sisi wenyewe. Wewe ni Ghana, mimi ni Ghana. Kwa pamoja tunaifanya nchi hii kuwa bora. Hebu tuingie katika agano la kujenga Ghana tunayotamani sote.” Alisema Dramani.

Alitoa wito kwa wananchi kuwa na maono ya Ghana wanayotaka kuiacha nyuma kwa ajili ya vizazi vijavyo, akihimiza mabadiliko ya mitazamo, tabia na fikra ili kufikia maendeleo ya pamoja.


 



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved