logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Serikali- pesa yote ya Inua jamii itatumwa na M Pesa

Serikali ya kenya imetangaza kuhamisha mpango wa pesa zote za inua jamii kufikia wananchi kupitia njia ya M Pesa.

image
na Japheth Nyongesa

Yanayojiri24 January 2025 - 16:15

Muhtasari


  •  Joseph Motari hapo jana Januari 23 alisema kwamba watu wote wanaonufaika na programu ya Inua Jamii watapokea mgao wao kupitia njia ya simu.
  • Ameeleza kwamba hilo litaanza kutendeka  kuanzia Januari hii na watazipata pesa hizo kupitia kubonyeza *222  kutumia laini ya kampuni ya Safaricom.


Serikali ya kenya imetangaza kuhamisha mpango wa pesa zote za inua jamii kufikia wananchi kupitia njia ya M Pesa. 

Katibu mkuu wa wizara husika  Joseph Motari hapo jana Januari 23 alisema kwamba watu wote wanaonufaika na programu ya Inua Jamii watapokea mgao wao kupitia njia ya simu.

Ameeleza kwamba hilo litaanza kutendeka  kuanzia Januari hii na watazipata pesa hizo kupitia kubonyeza *222  kutumia laini ya kampuni ya Safaricom.

"Watu wote wanaonufaika na Inua Jamii watatakiwa kuhakikisha laini yao ya m pesa imesajiliwa vilivyo kwa majina yao ili wapate pesa zao," alisema Motari.

Motari aliongeza kwamba wale ambao wana laini za safaricom wanafaa kuhakikisha ziko sawa na wale hawana wajisaji.

Amewataka wale ambao watashindwa wafike katika office ili kupata usaidi au wapige simu kupitia 1533, bila malipo ya hudhuma.

Baadhi ya ofisi ni kama; County/ Sub - county Social Development office, Sub-County Childrens Office, county Disability Offices.

Programu ya Inua Jamii sasa inawasaidia zaidi ya watu milioni1.7, wakiwemo watoto kutoka katika familia zisizojiweza, watoto  yatima, watu wenye mapungufu pamoja na watu wenye miaka 70 na kuendelea kutoka katika familia masikini. 

Pesa hizo huja kila mwezi ili kuwasaidia kupigana na lindi la umasikini na makali ya njaa.

Rais Wiliam Ruto akizungumzia hili siku chache zilizopita alisema kwamba fedha hizo kutumwa kupitia njia ya simu itasaidia pakubwa.Alisema kwamba imekuwa ikiwagharimu wahusika kusafiri kwa mwendo mrefu ili kufika kwenye benk kila mwezi jambo ambalo ni changamoto kubwa hasa kwa watu wenye umuri mkubwa.

Kulingana na takwimu za mwezi jana Serikali ilitoa bilioni 3.5 ili kuwawafikia watu watu milioni 1.5 kila mmoja akipata shilingi elfu mbili.




RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved