logo

NOW ON AIR

Listen in Live

DCI wamkamata mshukiwa kwa madai ya kumteka nyara mtoto wa miaka saba Kiambu

Mwanamme wa miaka 33 kwa jina Joseph Murith Kibutu alikamatwa na makachezo wa DCI kwa madai ya kumteka nyara mvulana wa miaka saba

image
na Evans Omoto

Yanayojiri19 February 2025 - 08:55

Muhtasari


  • Jambo hili liligundulika wakati ambapo wazazi wa mtoto huyo walipogundua kuwa mwanawe hayupo walipokuwa wakinunua bidhaa katika duka kuu la Savory mtaa wa Mwihoko.
  • Maafisa wa polisi  walilichukulia suala hilo kwa uzito na kuanzisha  uchunguzi wa haraka ili kumtafuta mhusika huyo na kumtoa mafichoni.

 Mshukiwa aliyemteka nyara Mtoto Kiambu

Mwanamme wa miaka 33  kwa jina Joseph Murith Kibutu alikamatwa na makachezo wa DCI kwa madai ya kumteka nyara mvulana wa miaka saba mtaa wa Mwihoko kaunti ya Kiambu mnamo Februari 17,2025.

Hii ilitokana na ushirikiano wa hali ya juu kati ya maafisa wa polisi wa  kituo cha Githurai  na maafisa wa DCI.

Jambo hili liligundulika wakati ambapo wazazi wa mtoto huyo walipogundua kuwa mwanawe hayupo walipokuwa wakinunua bidhaa katika duka kuu la Savory mtaa wa Mwihoko.Ghafla walitanabahi kupata mwanao hayupo licha ya juhudi za kumtafuta kugonga mwamba.

akiwa katika hali ya kuchanganyikiwa walipigiwa simu kutoka kwa mtu wasiye mfahamu   aliyesema kuwa yeye ndiye aliyekuwa na mwanao na kuitisha kitita cha shilingi elfu mia moja(100,000)  akiwahakikishia kuwa angemrejesha mwana kwa masharti ya kulipwa mwanzo.

Maafisa wa polisi  walilichukulia suala hilo kwa uzito na kuanzisha  uchunguzi wa haraka ili kumtafuta mhusika huyo na kumtoa mafichoni,kutokana na upelelezi wa hali ya juu mhusika huyo aliweza  kunaswa akiwa mafichoni maeneo ya  Githurai mtaa wa Reli.

Hatimaye walifanikiwa kumkamata mhusika Pamoja na mtoto ambaye alikuwa amefichwa na kumpokeza kwa wazazi wake akiwa salama,baada ya wazazi kumpata mwanao walijawa na furaha na kumshukuru Mungu kwa kuwaokolea mtoto wao.

Familia ilipokuwa ikifurahia kupatikana kwa mwanao na kusherehekea mshukiwa mkuu Joseph Murithi Kibutu alisalia korokoroni akifanyiwa ukaguzi na uchunguzi na mafisa wa Polisi huku akisubiri kufikishwa mahakamani kujibu mashitaka.

Ni tukio ambalo liliwaacha wengi vinywa wazi wakijiuliza maswali bila kupata majibu kuhusiana na jambo hilo, wengi wa wazazi walilaani kitendo hicho cha  kinyama huku wakiwahongera maafisa wa usalama kwa kukuwa ange na kumwokoa mtoto huyo.

Vilele wengi walielezea hofu ya usalama wa Watoto wao wakisema kuwa hilo tukio linaweka maisha ya familia nyingi katika hali ya wasiwasi wakisema ipo haja ya jamii kushirikiana na kuwatambua watu walio na nia mbaya kama ya bwana Murithi.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved