logo

NOW ON AIR

Listen in Live

DCI yachunguza kisa cha wizi wa kimabavu kinachohusisha police wawili

Idara ya DCI imeeleza kwamba maafisa hao wawili ndio washukiwa wakuu baada ya kufumaniwa katika shughuli za kumunyanyasa raia kwa usaidizi wa mhusika wa tatu katika mtaa wa Githura

image
na Japheth Nyongesa

Yanayojiri19 February 2025 - 09:07

Muhtasari


  • Waliwatia mbaroni wahusika hao ambao walitambulika kama maafisa wa usalama pamoja na muhusika wa tatu.
  • Maswala ya vyombo vya usalama kuhusika katika vitendo viovu vya kuwabia wananchi badala ya kuwalinda na mali zao vinaongeza wasiwasi miongoni mwa wananchi.

Maafisa wawili wa  polisi wametiwa mbaroni huku uchunguzi ukianzishwa kwa tuhuma za kuhusika katika wizi wa kimabavu jijini Nairobi.

Idara ya DCI imeeleza kwamba maafisa hao wawili ndio washukiwa wakuu baada ya kufumaniwa katika shughuli za kumnyanyasa raia kwa usaidizi wa mhusika wa tatu katika mtaa wa Githurai.

Kulingana na repoti ya polisi, Maafisa wa usalama wa Gidhurai wakiwa kwenye shughuli zao za kawaida ndipo walipowafumania maafisa hao waliokuwa wakimuibia raia.

Waliwatia mbaroni wahusika hao ambao walitambulika kama maafisa wa usalama pamoja na muhusika wa tatu.

Watatu hao walikuwa wamemwangusha raia huyo chini wakiwa na nia ya kumuibia bidhaa zake' Tayari wamefikishwa kwenye kituo cha police cha Gidhurai wakingoja kufikishwa mahakamani.

Kulingana na kitendo hicho idara ya DCI imewaonya raia na maafisa wa usalama kushirikiana katika kuwaibia watu, idara hiyo imesisitiza kwamba vitendo kama hivyo vitachukuliwa na sheria kali sana.

Kitendo hiki kimetokea siku chache tu baada ya maafisa wa  kitengo cha Serious Criminal investigation [SCU[ kwa kushirikiana na wengine kumutia mbaroni afisa ya DCI anayedaiwa kuhusika katika wizi wa kimabavu.

Afisa huyo wa DCI, kutoka Kibwezi Kaunty ya Makueni alishikwa siku ya Jumaa tatu Feburuari 17 kutokana na ushahidi unaomuhusisha na wizi wa kimabavu mwaka 2022'

Wakati wa wizi huo mhudumu mmoja alipigwa risasi tumbuni na kuaachwa akiuguza majeraha kabla ya mshukiwa kotoroka na shilingi elfu 50.

Maswala ya vyombo vya usalama kuhusika katika vitendo viovu vya kuwabia wananchi badala ya kuwalinda na mali zao vinaongeza wasiwasi miongoni mwa wananchi.

Hili ni jambo ambalo idara husika zinafaa kushugulikia kwa kina na kukomesha kabisa ili kuleta imani katika vyombo vya usalama kwa wananchi.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved