logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Maraga asikitikia hali ya Afya nchini

Aliyekuwa Jaji mkuu David Maraga alielezea wasiwasi wake kuhusu hali mbaya inayoendelea katika hospitali za umma nchini.

image
na Evans Omoto

Yanayojiri21 February 2025 - 10:07

Muhtasari


  • Maraga alisema kuwa kutozipa hela hospitali hizo hakustahiki ikizingatiwa kuwa serikali i mbioni kuvumisha mfumo wa huduma za afya kwa jamii kwa wote  ambao unastahili kuwa unawajibikia suala hilo pana.

Jaji mkuu wa zamani Maraga ahimiza serikali kuzingatia Afya

Aliyekuwa Jaji mkuu David Maraga alielezea wasiwasi wake  kuhusu hali mbaya inayoendelea katika hospitali za umma nchini.

Katika chapisho rasmi aliloandika katika ukurasa wake wa X uliojulikana kama twita jaji  huyo wa Zamani alisikitikia wito wa muungano wa hosiptali za binafsi wa kutaka kusitisha huduma zake kwa wagonjwa kwa kisingizio cha serikali ya taifa kutolipa malimbikizi ya madeni kwa hospitali hizo.

Maraga alisema kuwa kutozipa hela hospitali hizo hakustahiki ikizingatiwa kuwa serikali i mbioni kuvumisha mfumo wa huduma za afya kwa jamii kwa wote  ambao unastahili kuwa unawajibikia suala hilo pana.

Alisema kuwa Wakenya wengi walikuwa wakitoa pesa kwa huduma za NHIF mwanzoni kabla ya kuhamia kwa huduma ya SHA alisema kuwa ni hatua ya wagonjwa kunyimwa huduma za matibabu ambayo ni haki yao kimsingi haistahili.

Alikariri kuwa wagonjwa wengi huhitaji huduma za dharura ikikusudiwa  kuwa maradhi wanayokabiliwa nayo hayawezi kusubiri kamwe.

Alitoa wito kwa serikali kuchukua hatua za haraka kusuluhisha suala hilo na kuokoa sekta ya afya ambayo ni nguzo muhimu katika maisha ya binadamu vilevile aliongezea akisema kuwa afya ni jambo la tija katika maisha  ya mja yeyote hivyo basi linasitahili kushughulikiwa  kwa dharura.

Alisema kuwa idara ya afya kutotoa huduma bora kwa umma imetekwa na sheria  mbovu ambazo hazisaidii na vilevile ufisadi ambao umeshehemni na kumea zaidi .

Alisema kuwa kama taifa hatuwezi kuwa tunapiga hatua mbili mbele na tunapiga hatua tano nyuma kimaendeleo kama taifa, kwa idara ya afya linakuwa ni jambo la kufedhehesha sana kwa sababu  ya watu wachache kupata nafasi ya kupora pesa za umma.

Maraga alisema kuwa taifa ambalo lina watu wagonjwa haliwezi kupiga hatua kimaendeleo na kufikia ruwaza inayolenga hivyo ni jukumu la serikali kuhakikisha kuwa tiba katika nchi iko imara na ya kujivunia ipasavyo.

Kauli ya Maraga inajiri wakati ambapo madaktari wanashinikiza serikali kuwalipa madaktari wanagenzi mishahara yao.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved