logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Spika wa Turkana Christopher Nakuleu ajiuzulu

Nakuleu alijiuzulu siku mbili kabla ya mswada wa kumuondoa mamlakani kujadiliwa.

image
na Japheth Nyongesa

Yanayojiri26 February 2025 - 12:15

Muhtasari


  • Nakuleu alisema amefanya  mashauriano mapana na wapiga kura  na wafuasi wake katika Kaunti nzima, ndipo akafikia hauta ya kujiuzulu.
  • Nakuleu alimtaka Gavana aeleze kwa undani, mbona baadhi ya bidhaa hazikuwasilishwa kulingana na bajeti iliokuweko.

Spika wa kaunti ya Trukana Christopher Doye Nakuleu alijiuzulu Jumanne siku mbili kabla ya kujadiliwa mswada wa kumuondoa mamlakani kujadiliwa.

Mwakilishi wadi wa Kalolok Michael Ebenyo aliwasilisha bungeni mswada wa kumbandua ofisini spika huyo kutokana na madai ya utovu wa nidhamu.

Kulingana na Nakuleu, alieleza kwamba amefanya  mashauriano mapana na wapiga kura  na wafuasi wake katika Kaunti nzima, ndipo akafikia hauta ya kujiuzulu.

"Ninaandika kujiuzulu rasmi kutoka nafasi yangu kama spika wa Bunge la Kaunti ya Turkana kuanzia Februari 25, 2025. Nimepata uzoefu wa thamani na kuunda uhusiano wa maana wakati wa mamlaka yangu. Uamuzi huu unakuja baada ya kuzingatia kwa makini malengo yangu binafsi na ya kitaaluma,"sehemu ya barua yake ilisoma.

Kujiuzulu kwake kunatajwa kama hatua ya busara kwani anapanga  kujiandaa ili kupigania nafasi ya ugavana katika kauniti hiyo ili kumuondoa gavana wa sasa Jeremiah  Ekamais Lomorukai mamlakani.

Wiki jana, angalau  wawakilishi wadi wapatao 36 kati ya 46 waliunga mkono ombi lililowasilishwa kama hoja maalum ya kumuondoa spika madarakani sababu kuu zikitajwa kama ukiukaji wa katiba, utovu wa nidhamu na kutowajibika.

Kumekuwepo na madai kwamba uhusiano kati ya Nakuleu na Gavana wa kaunti hiyo ulianza kuzorota baada spika huyo kutaka kujua jinsi Fedha zilizokuwa zimetengwa ili kusaidia kununua chakula cha msaada kwa wenyeji zilivyotumika.

Nakuleu alimtaka Gavana aeleze kwa undani, mbona baadhi ya bidhaa hazikuwasilishwa kulingana na bajeti iliokuweko.

 "Jukumu langu ni kusimamia na kuangalia utendaji. Bunge la Kaunti lilitenga milioni 551 kwa ajili ya ununuzi wa shehena kamili ya chakula cha msaada ikiwa ni pamoja na mahindi, maharagwe na mafuta ya kupikia mboga lakini hakuna maharagwe yaliyoletwa." alisema spika huyo, awali.

"Nyote mnafahamu kuna fumbo Turkana na jamhuri ya Kenya kuhusu sakata ya chakula cha msaada ambapo gavana hadi sasa hajatoa majibu kuhusu maharage hayo. Bosi wa Kaunti lazima awaambie watu wa Turkana mahali ambapo pesa za misaada zilikwenda." aliendea.

Kwa upande wake Gavana Lomorukai ametaja tetesi hizo kama propaganda za kisiasa tu. Alieleza kwamba walinunua magunia 119,000 ya mahindi na mafuta ila fedha hazikutosha kununua maharagwe.

"Kile ambacho spika anataka ni siasa za bei rahisi. Hatukuweza kujumuisha maharage katika bajeti ya chakula cha msaada kwa sababu MCAs walipunguza bajeti iliyopendekezwa kutoka milioni 700 hadi  milioni 551,' alisema Gavana.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved