Wizara ya Ulinzi yakanusha taarifa zilizochapishwa katika
magazeti ya Sunday Nation na Taifa leo kuwa Raila Odinga aliokoa Rais Ruto kutoka
nchi kuchukuliwa na Jeshi kufuatia maaandamano ya vijana wa Gen -Z Ya kupinga msuada
wa Fedha wa 2024-2025.
‘’ Wizara ya Ulinzi ingependa kukanusha na kusema kuwa
taarifa zilizochapishwa katika magazeti ya vyombo vya Habari ya Sunday Nation
na Taifa Leo mtawalia yaliyokuwa na Mada
nikinukuu RAILA: ‘’I saved Ruto from
Millitary Coup’’ na Gazeti la Taifa
Jumapili lenye mada ‘’Nilivyozima
Mapinduzi Dhidi ya Ruto’’.
Barua hio ilioeleza kuwa machapisho hayo katika magazeti ya taifa hayakueleza na
kufafanua vyanzo maalum vya madai hayo kuwa aliyekuwa Waziri mkuu wa Zamani Raila
Odinga katika mahojiano yake na vyombo vya kuwa alizuia uongozi wa Rais Ruto
dhidi ya kuchukuliwa na Majeshi.
Wizara ya ulinzi wa taifa
la Kenya ilitaja Habari hizo kama za uongo,hazina msingi,zizizokuwa na
Mashiko ,Habari za Kupotosha na za kimzaha .
Kupitia kwa barua hiyo ujumbe ulizidi kueleza kuwa Wizara ya
ulinzi ni taasisi ambayo ina maadili na ambayo ilijitolea kufanya kazi kwa
heshima ,maadili na kutumikia taifa kwa haki,usawa na uwazi.
Jeshi la taifa litasalia kuwa imara na tiifu kwa Rais ambaye
ni amri jeshi mkuu wa majeshi yote ya
taifa na liko imaara na tayari kwa kulinda taifa kwa hali na mali
pasi kuegemea mirengo ya kisiasa au kuwa na masilahi ya binafsi.
Machapisho ya Taifa Leo na the Sunday Nation yalitoa taarifa
zisizo za kweli na ambazo vyanzo vyake havithaminiki ifaavyo na lengo la machapisho hayo yalikiuka uzalendo wa
nchi na kujikita katika lengo la kuongeza idadi ya wasomaji huku yakikwepa ustaarabu wa wanahabari
inavyostahiki.
Hivyo wizara ya ulinzi ilitoa wito kwa mashirika ya vyombo
vya Habari kuzingatia ukweli na maadili na vilevile usalama wa taifa haswa wanaporipoti
masuala kuhusu usalama wa taifa barua
ilifafanua kwa undani zaidi.
Wizara ya ulinzi inatoa taarifa ya kukanusha madai haya siku
moja baada ya magazeti hayo kuchapishwa
ambapo mhusika mkuu bwana Raila Odinga alihojiwa siku ya Jumamosi katika
mahojiano yalifanyika nyumbani kwake Karen.