logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mkazi wa Nakuru amtaka Gavana Kihika arudi nyumbani kutoka Marekani

Mkaazi wa Nakuru anashurutisha Gavana Kihika kurudi nyumbani baada ya kukaa sana katika taifa la Marekani.

image
na Evans Omoto

Yanayojiri25 March 2025 - 14:31

Muhtasari


  • Katika barua kwa rais wa Marekani Donald Trump na kwa Rais wa Kenya William Ruto Evans  Kimori katika barua yake alisema kuwa taifa la Marekani lifanikishe kurudi kwake nyumbani ili aendeleze majukumu yake kama Gavana.
  • Alisema kuwa wakazi wa NAKURU  wanahitaji uwajibikaji wa uongozi hata hivyo walisisitiza kuwa kutokuwepo kwa Gavana Kihika kunawanyima  haki ya kupata uongozi mwema kutoka kwa wapiga kura.

Mkaazi wa Nakuru anashurutisha  Gavana  Kihika kurudi nyumbani baada ya kudaiwa kukaa sana katika taifa la Marekani.

Katika barua kwa rais wa Marekani Donald Trump na kwa Rais wa Kenya William Ruto Evans  Kimori katika barua yake alisema kuwa taifa la Marekani lifanikishe kurudi kwake nyumbani ili aendeleze majukumu yake kama Gavana.

''Kwa niaba ya watu wa Nakuru kwa heshima ninaomba uingilie kati kwa kuhakikisha kuwa Bi Kihika anarudishwa nyumbani Kenya ili aendeleze shughuli zake za kikazi,'' barua ya Bwana Kimori ilisema.

Alisema kuwa wakazi wa Nakuru  wanahitaji uwajibikaji wa uongozi hata hivyo walisisitiza kuwa kutokuwepo kwa Gavana Kihika kunawanyima  haki ya kupata uongozi mwema kutoka kwa wapiga kura.

Vilevile Kimori alimkashifu Bi Kihika kwa kuifunga Hospitali ya War Memorial ambayo alisema iliwaacha mamia ya wakazi wa Nakuru bila huduma za afya njema jambo walilokuwa wakipata hapo mwanzoni.

Alisisitiza kuwa kuendelea kukaa kwa Gavana Kihika Katika Taifa la Marekani ni kuashiria kuwa anakwepa majukumui yake  ilihali anaendelea kupokea mshahara mnono kutoka kwa walipa ushuru wa Kenya hasa wakazi wa Nakuru.

''Kama kiongozi aliyechaguliwa kama Gavana ana haki ya kikatiba kuhakikisha kuwa anafanyia kazi wananchi waliomchagua kazi kama vile Huduma za afya  ambayo ni tija kuu kwa wananchi ilihali yeye kukaa kwake sana Marekani ilihali huduma muhimu zinaendelea kuyumbayumba  inaonyesha ukiukaji mkubwa wa kazi kwa wananchi ilihali anaendelea kupata mshahara mkubwa''. Bwana  Kimori alilama katika barua yake.

Wakati ambapo chapisho hili lilikuwa linachapishwa  hakukuwa na majibu kwa barua ya bwana kimori kutoka kwa wahusika waliotajwa katika barua rais  TRUMP NA RUTO ilihali Gavana mwenyewe alionekana akituma miradi ya maendele,o inayoendelea katika gatuzi lake la Nakuru.

'' Kwa siku chache zilizopita tumeendelea kutoa huduma  za maendeleo kwa kuangazia miradi mbalimbali ya Maendeleo ya maji na kuendeleza ustahimilivu  wa hali ya tabianchi kupitia kwa kufadhili mradi wa tabianchi wa FLLOCA ''. bi Kihika alieleza.

Mnamo Machi 11,2025 Milicent Omanga aliwahi tuma picha ya wao wakiwa wawili ila hakufafanua  wala kusema zaidi ni wapi walipokuwa na walikuwa wakifanya nini. 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved