logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Raila Odinga asema ODM haiko katika serikali

Raila Odinga akanusha vikali kuwa chama chake cha ODM kuwa ndani ya serikali akisema kuwa aliipa serikali wataalamu wa kuchapa kazi.

image
na Evans Omoto

Yanayojiri27 March 2025 - 07:49

Muhtasari


  • Odinga alizungumza hayo akiwa katika matanga ya marehemu Julius Laban Murungi  Kule Meru ambaye ni babake Betty Murungi Orengo ambaye ni mkwe wake Gavana wa Siaya James Agure Orengo.
  • Katika hafla hiyo bwana Odinga  aliweza kufafanua wazi kwa kusema kuwa yeye pamoja na chama chake hawako katika serikali ya KENYA KWANZA bali waliweza tu kushirikiana nayo kwa manufa ya ustawi wa taifa.

Raila Odinga akanusha vikali kuwa chama chake cha ODM  kuwa ndani ya serikali akisema kuwa aliipa serikali wataalamu wa kuchapa kazi.

Odinga alizungumza hayo akiwa katika matanga ya marehemu Julius Laban Murungi  Kule Meru ambaye ni babake Betty Murungi Orengo ambaye ni mkwe wake Gavana wa Siaya James Agure Orengo.

Katika hafla hiyo bwana Odinga  aliweza kufafanua wazi kwa kusema kuwa yeye pamoja na chama chake hawako katika serikali ya KENYA KWANZA bali waliweza tu kushirikiana nayo kwa manufa ya ustawi wa taifa.

Odinga aliweza kusema kuwa kutokana na wimbi lililokuwa likikabili serikali ya Kenya Kwanza kutokana  na maandamano ya vijana wa kizazi cha  Gen z ni baadhi ya sababu kuu  zilizofanya ajitolee aisadie  serikali ya Kenya kwwanza na wataalum wa kazi  ili taifa liweze kusonga mbele.

''Wakenya walisema Ruto ni Lazima aende, wakapinga mswada wa fedha wa 2024/2025 hatimaye alikuja akawasikiliza na kuvunjilia mbali baraza lake la mawaziri hatimaye aliniomba nimpe wataalamu wa kazi, tumemsaidia tu Chama cha ODM hakipo kwa serikali , Mimi si waziri katika serikali ya Ruto''. Odinga alieleza.

Shinikizo hizo zilizidi kutolewa kutokana na chama hicho cha ODM kuweza kutoa zaidi ya mawaziri watano John Mbadi wa Fedha,Dorcas Oduor  mshauri mkuu wa serikali, Opiyo Wanayi waziri wa Nishati,Wycliffe Oparanya waziri wa Mashirika na biashara ndogondogo na Hassan Joho  Waziri wa madini na uchumi wa majini miongoni mwa makatibu wakuu katika wiraza mbalimbali walioteuliwa muda mchache uliopita.

Hata hivyo kutokana na uwepo wa wafanyakazi hawa kutoka ODM ndani ya serikali ndio uliochochea watu kuamini kuwa ODM iko katika serikali ya Kenya Kwanza na hivyo kuwa inacheza karata mara mbili kuwa katika serikali na kwa wakati huo kusema wako upinzani.

Kiongozi wa Chama cha People Liberation Party Martha Karua ambaye pia alikuwa muwaniaji mwenza wa Odinga katika Uchaguzi uliopita wa 2022 alimkashifu Odinga kwa  kuwa ndumakuwili kuwa ndani ya serikali na vilevile kujidai kuwa wako upinzani. 

Aliweza kusema kuwa itakuwa vyema kama Serikali ya Kenya kwanza na ODM watafika katika afisi za msajili wa vyama ili waihalalishe ndoa yao rasmi ili kusiwe na mchanganyiko unaoshudiwa nchini hata mpaka kwenye bunge la Taifa ambapo mahakama ilitoa uamuzi kwa kusema kuwa mrengo wa Azimio ndio ulio na idadi kubwa ya Wabunge jambo ambalo Spika wa bunge la Taifa Moses Masika Wetangula alisusia kutii agizo hilo hadi sasa.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved