logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Gachagua aliandaa wakazi wa Mlima Kenya kuhusu ziara ya rais - Seneta Joe Nyutu

Seneta wa Muranga alidai kuwa aliyekuwa Naibu wa Rais Rigathi Gachagua alikuwa amewapanga mapema.

image
na Evans Omoto

Yanayojiri03 April 2025 - 10:30

Muhtasari


  • Katika maelezo yake Bwana Nyutu alisema kuwa Gachagua alikuwa tayari amewaelezea wakaazi wa Mlima Kenya kuhusu uwezekano wa Rais kuweza kuwashawishi wakazi wa mlima kenya kwa maneno matamu.

Joe Nyutu

Seneta wa Muranga Joe Nyutu amedai kuwa aliyekuwa Naibu wa Rais wa Ramani Rigathi Gachagua alikuwa amewapanga wakaazi wa Mlima Kenya kuhusu ujio wa Rais Ruto Mlimani..

Katika maelezo yake Bwana Nyutu alisema kuwa Gachagua alikuwa tayari amewaelezea wakaazi wa Mlima Kenya kuhusu uwezekano wa Rais kuweza kuwashawishi wakazi wa mlima kenya kwa kuwaelezea maneno matamu kuhusu ziara yake ambayo alikuwa amekusudia kuitekeleza.

'' Naibu wa Rais wa pili bwana Rigathi Gachagua alikuwa amewashauri watu wetu kuwa kulikuwa na pesa ambazo zilikuwa zinasitahili kupelekwa kwa wizara ya Elimu, wizara ya afya(SHA),na kuwapelekea watoto wetu Nyumbani  lakini hizi pesa zimegeuzwa kutoka kwa kushughulikia vitu muhimu''.Nyutu alisema.

''Tuliwashauri kutochukua hela chache kwa sababu kulikuwa na zawadi ya  pesa  nyingi ilikuwa inawangoja  kwa kuhudhuria mikutano  zawadi ya kupiga makofi na kutabasamu na  hivyo ndivyo Rais Ruto alivyofanya.'' Seneta Nyutu alieleza.

Matamshi ya Nyutu yanajiri wakati ambapo  Kiongozi wa taifa kwa sasa anaendeleza ziara yake kwa siku ya Tatu akiwa katika eneo pana la  Mlima Kenya kwa ajili ya uzinduzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo. 

Rais  siku ya leo anatarajiwa kuzuru Kaunti ya Nyandarua na hatimaye kufululiza moja kwa moja hadi kaunti ya Muranga kwa msururu wa kuzindua miradi mbalimbali ya maendeleo.

Itakumbukwa wazi kuwa kabla Rais aanze ziara yake Mlimani aliyekuwa Naibu wa Rais Rigathi Gachagua alikuwa  amewarai wakaazi wa Mlima Kenya Kumuuliza rais ni maendeleo gani aliokuwa anaenda kuzindua ilihali barabara nyingi na miradi mingi ilikuwwa imekwama.

Vilevile Naibu huyo wa rais alikuwa amekisia kuwa kutokana na kuondolewa kwake katika serikali wakaazi wa Mlima Kenya walikuwa hawana imani na rais kwa kiwango kikubwa hivyo alikuwa ametoa madai kuwa wananchi wangelipwa pesa nyingi ili waweze kuhudhuria mikutano yake.

Lakini  kinyume cha matarajio ya wengi tangu wakati ambapo rais alipotua katika eneo hilo hasa  kaunti ya  Laikipia na Nyeri  wananchi wengi walijitokeza kushiriki na kuhudhuria mikutano yake  huku wakimshangilia kwa shangwea na nderemo.

Hata mwandani wa karibu wa Rigathi Gachagua bwana Mutahi Kahiga gavana wa Nyeri alikuwa mstari wa mbele kumpokea rais kwa mikono miwili.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved