logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Serikali kukata rufaa kuhusu uamuzi wa mahakama kuu dhidi ya ulipaji karo kupitia E -citizen

Serikali ilitangaza azma yake ya kukata rufaa kutokana na uamuzi wa mahakama kuhusu malipo ya E -citizen

image
na Evans Omoto

Yanayojiri03 April 2025 - 08:06

Muhtasari


  • Katibu mkuu katika wizara ya elimu Julius Bitok alisema hayo alipokuwa katika mtaa wa Mkuru kwa  Njenga walipokuwa wakizindua mradi wa madarasa mapya manane pamoja na mijengo mingine mitatu.
  • Katibu Bitok Katika hotuba yake aliweza kuihongera serikali ya Marekani kupitia kwa balozi  wake hapa nchini Marc Dillard  ambapo takribani shilingi  milioni 84 ziliweza kutolewa kufadhilimpango huo.

Serikali imetangaza azma  yake ya kukata rufaa  kutokana na uamuzi wa mahakama kuu ya kusitisha  malipo  katika mfumo wa E-citizen katika shule .

Katibu mkuu katika wizara ya elimu Julius Bitok alisema hayo Jumatano alipokuwa katika mtaa wa Mukuru kwa  Njenga walipokuwa wakizindua mradi wa madarasa mapya manane pamoja na mijengo mingine mitatu.

Mradi huo uliweza kufadhiliwa na serikali ya Merekani kupitia kwa wizara  ya ulinzi kwa  ushirikiano na serikali ya Kenya kupitia kwa wizara ya elimu kwa programu ya Endeleza elimu katika Jamii.

Katibu Bitok Katika hotuba yake aliweza kuihongera serikali ya Marekani kupitia kwa balozi  wake hapa nchini Marc Dillard  ambapo takribani shilingi  milioni 84 ziliweza kutolewa kufadhilimpango huo.

Kutokana na mchango huo kulipa nafasi idara yetu ya elimu kuweza kuimarisha misingi yake  na  kuhakikisha kuwa kila kitu kinakwenda kwa uzuri na kwa manufaa ya wanafunzi na jamii kwa jumla.

''Maisha yetu ya siku za baadaye yanategemea elimu ya watoto wetu,kwa hivyo ushirikiano wetu na mashirika kama haya ambayo tunafurahia  siku ya leo yanafaa kuwekwa juu kwa manufaa ya kusaidiana katika kila upande, kufikia sasa serikali ya taifa imejenga zaidi ya madarasa 16,000 ya gredi ya 9 kote nchini, Shule hii ya Kwa Njenga ni moja kati ya shule zitakazokuwa miongoni mwa shule bora nchini''.Bitok alisema katika hotuba yake.

Hata hivyo mpango huo ulipokuwa ukiendelea bwana Bitok  aliweza kutoa tangazo kuwa serikali kupitia kwa wizara ya elimu itafika mahakamani kwa ushirikiano na afisi ya mshauri mkuu iili kuweza kukata rufaa kutokana na uamuzi wa mahakama kuu kuweza kusimamisha ulipaji wa Karo kwa kutumia mfumo wa E-CITIZEN.

Siku ya Jumanne jaji Chacha Mwita wa mahakama kuu aliweza kutoa uamuzi wa kusitisha ulipaji karo kwa kutumia mfumo wa e citizen Jaji alisema kuwa hakukuwa na ushirikishi wa umma ipasavyo kabla ya kuafikia kiwango cha utekelezaji wake.

Itakumbukwa wazi kuwa aliyekuwa katibu mkuu wa wizara ya elimu Belio Kipsang alikuwa ametoa mwongozo kwa shule zote kuwa  zifanye malipo kwa e -citizen.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved