
Aliyekuwa naibu wa rais Rigathi Gachagua amesema kuwa maovu yaliotendeka miaka ya nyuma ya 2007 na 2008 makanisani yanajitokeza tena mwaka
Gachagua alisema kuwa mnamo mwaka wa 2007 baada ya uchaguzi mkuu kulitokea machafuko ya ghasia za kikabila ambapo watu wengi waliweza kupoteza makao halikadhalika na maisha yao.
Gachagua aliweza kusema kuwa kulitokea magenge ya wahuni mwaka wa 2007/2008 waliokuwa wakiwauwa watu na kuwakatakata na vilievile kuchoma makazi yao kama vile tukio lililotokea katika kanisa la Kiamba ambapo watu wengi waliweza kuuwawa kwa kuchomwa moto.
Gachagua alikuwa akisimulia kisa hicho cha kumbumbuku ya zamani kwa kuweza kuvuta taswira na kurejelea hali halisi ya matukio yaliofanyika katika eneo la Kasarani alipokuwa akihudhuria ibaada ya maombi katika kanisa la PCEA Mwiki siku ya Jumapili ya tarehe 6 Aprili ,2025.
Mnamo Jumapili ya tarehe 6 Machi,2025 Gachagua akiwa katika kanisa la PCEA Mwiki Kasarani kulitokea kundi la vijana waliovamia waumini kanisani na kutaka kusambaratisha ibaada iliyokuwa ikiendelea na vilevile kutaka kulipwa hela kwa lazima.
Gachagua alikuwa ni mwingi wa masikitiko akijutia kwa kusema kuwa anashangaa kuona matukio yaliyofanyika zaidi ya miaka kumi na tano iliyopita ikijirudia tena ya visa vya uhalifu na ugaidi makanisani.
''Mwanzo nina masikitiko makubwa sana kuweza kushuhudia matukio tulioona ya mwaka wa 2007 na 2008 ya uhalifu wa watu kuvamiwa makanisani ambapo watu wengi sana waliweza kuuuwawa kwa kuchomwa moto wakiwa kanisani Kule Kiamba'' Bwana Gachagua alisema.
'' Katika tukio hilo kulikuwa na akina mama na watoto wao wakati ambapo wahuni hao waliwavamia na kwa kuwa wanataka kuwauwa wakiwa kanisani wale kina mama waliweza kuzai kwa kusema kuwa ni vyema wao wauawe na ilihali waache watoto wakiwa hai ila walisusia na kuweza kuwasha moto na kuchoma kanisa zima watu wakiwa ndani huku watoto hao wakirushwa ndani kupitia kwa madirisha''.Gachagua alieleza.
Gachagua aliweza kusema hayo akirejelea tukio lililomtendekea akiwa Mwiki Kasarani akihudhuria ibaada alisema kuwa kwa kufanya hivyo wanawakumbusha wale waliokumbwa na machafuko hayo kuwa uhasama wa kijamii na vita makanisani vingalipo jambo ambalo aliomba serikali kutoruhusu kwa vyovyote vile.