logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mbunge Evance Kamange apuuzilia mbali madai ya wabunge wengi wa CCM kuhongana ili kupata kiti

Wabunge wengi wa chama cha CCM walishiriki hongo katika uchaguzi mdogo wa ngazi ya maeneobunge

image
na Evans Omoto

Yanayojiri14 April 2025 - 11:23

Muhtasari


  • Evance Kamange  mbunge  wa chama cha Mapinduzi  Tanzania CCM alikiri kuwa wabunge wengi  wa CCM waliingia bungeni kwa  kutumia Rushwa.

Evance Kamange,  mbunge  wa chama cha Mapinduzi  Tanzania CCM, ameweka wazi kuwa wabunge wengi  wa CCM waliingia bungeni kwa  kutumia Rushwa.

 Kamange alikuwa akizungumza na mwanahabari Chief Odembo Aprili 14,2025  alisema kuwa  katika uchaguzi wa  mwaka wa 2020 katika uchaguzi wa mchujo wabunge wengi wa CCM hawakupita kwa haki.

 Kamange  aliendelea kwa  kusema kuwa  katika kipindi hicho cha  uchaguzi wa  mchujo wabunge wengi  walitumia pesa zao kuweza kujinyakulia nafasi za  uongozi kwa sababu kulikuwa na idadi ndogo ya wapigakura  ambao hawangewawezesha kujinyakulia ushindi wa moja  kwa moja.

''Mwaka wa 2020 katika  uchaguzi wa chama cha ndani uligubikwa na rushwa mimi mwenyewe  nilikuwepo na nilishuhudia hilo , kuna baadhi ya  wabunge ambao walichukua uongozi ambao hawana maono  ya kumtetea mwananchi  na kuweza kutekeleza mambo kwa faida ya mwananchi.

 Baadhi ya wabunge  walichaguliwa tu kwa ajili ya uwezo wao wa hela  na  walizidi kumpongeza rais  badala  ya kujenga mifumo miema  ya kuweza kumsaidia mwananchi wakiwa kule  bungeni ili  waweze kuangazia matatizo ambayo yalikuwa yakimsonga mwananchi mpiga  kura. 

 Kwa  mfano wewe  kama mbunge  unastahili kuwa  na akili pevu tena tambuzi ya  kuweza kuwa na uongozi mwema ambao   wapiga kura  waliokuchagua  ni kwa ajili ya kuwasilisha miswada kule  bungeni ya  kumtetea  na  kumlinda  mwananchi wa kawaida  lakini  miongoni mwa  viongozi  hawa  waliochaguliwa hawana  wazo hilo wala uwezo wa  kulandana  na mabadiliko ya kileo katika kuandaa  miswada mbalimbali'' Kamange  alieleza.

Unajihisi vipi wewe kama kiongozi ambaye  alichaguliwa  katika chama tawala cha CCM  ila unahisi kuwa mmoja yule  ambaye  ulichaguliiwa kwa misingi au kwa  nguvu za hongo pamoja na wabunge  wengine?

 '' Kwa hakika sihisi vibaya ila ninataka kuwa mhimili wa mabadiliko katika uongozi wa  chama cha CCM kwa hivyo ninataka kuwa  kiongozi wa  mabadiliko katika uongozi  wa kisisa  hivyo mabadiliko ya shareia za chama ni mazuri ili kuzingatia haki na ukweli pia ni jambo jeme.''

 Matukio hayo yanajiri muda mchache wakati amabapo  chama cha upinzani  cha chadema kilipigwa marufuku kuweza  kushiriki katika  uchaguzi mkuu wa mwaka wa 2025.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved