logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Rigathi Gachagua adai maisha yake yako hatarini

Aliyekuwa naibu wa Rais Rigathi Gachagua aliandika barua ya kusema kuwa maisha yake yalikuwa hatarini na alihitaji ulinzi

image
na Evans Omoto

Yanayojiri15 April 2025 - 09:31

Muhtasari


  • Gachagua aliandika  barua hiyo mnamo APRILI 15 , 2025 iliyoelekezwa kwa inspekta mkuu wa  polisi bwana Douglas Kanja.
  • Kulingana na  bwana Gachagua alisema kuwa  kulingana  na kuondolewa kwa usalama wake  alisema kuwa maisha yake  yalikuwa hatarini  pamoja na familia yake  na wafuasi wake.

Rigathi Gachagua

Aliyekuwa naibu wa Rais Rigathi Gachagua aliandika barua ya kusema kuwa maisha yake  yalikuwa hatarini na  alihitaji kurejeshewa maafisa wake wa ulinzi.

Gachagua aliandika  barua hiyo mnamo APRILI 15 , 2025 iliyoelekezwa kwa inspekta mkuu wa  polisi bwana Douglas Kanja.

Kulingana na  bwana Gachagua alisema kuwa  kulingana  na kuondolewa kwa usalama wake  alisema kuwa maisha yake  yalikuwa hatarini  pamoja na familia yake  na wafuasi wake.

Alisema kuwa kulingana na  hitaji la katiba ya Kenya kila mtu  ana haki ya kulindwa pamoja na mali yake  ila akamnyoshea inspekta mkuu wa  polisi Douglas Kanja  kidole  cha lawama kwa kutuia jicho hali hiyo.

 Gachagua   katika maelezo yake  alisema  kuwa insipekta mkuu wa  polisi hakustahili kuegemea upande  wowote kulinganna na hitaji la  katiba  kifungu 245 (b) cha katiba ambapo afisa wa polisi hafai kuegemea upande  wowote anapotekeleza wajibu wake.

Gachgua  aliendeleza mfulilizo wa lawama kwa inspekta mkuu wa polisi kwa  kuwa  mstari wa mbele kushirikiana  na kuwaruhusu wahuni kumuhujumu na kuaribu mali ya  thamani ya pesa  nyingi ilihali vyombo vya dola vilikuwepo vikitazama  tu.

Alielezea kisa  cha mnamo Novemba 28, 2024 alipokuwa katika hafla  ya matanga Limuru  aliweza kuvamiwa na magenge  ya wahuni huku thamani ya vitu vingi vikiharibiwa. 

 Gachagua  aliendeleza msururu wa maelezo kuhusu  kuvamiwa kwake   katika hafla tofauti tofauti za  maombi  katika mikutano yake  ya  kisiasa.

 Alisema kuwa mnamo Desemba 28,2024 akiwa katika Kaunti ya Nyandarua aliweza kurushiwa  kitoza machozi mbele ya maafisa wa usalama akisema kuwa tukio hilo bila shaka lilikuwa ni tukio la kumtoa uhai.

Alipokuwa katika Kaunti ya Nyeri mnamo 18 January,2025 katika uwanja wa Kamukunji akiwa  Nyeri Mchumba wake  bi Doroth Gachagua aliweza kuvamiwa na genge la wahuni waliosambaratisha huduma za  mkutano wa kanisa uliokuwa ukiendelea.

Mnamo 23 Machi,2025 akiwa katika kanisa la ACK  Cathedral Nyeri magenge  ya wahuni  yalianza vurugu na hali ya wasiwasi huku wakiwakandamiza waumini .

Kutokana matokeo haya  na mengine Gachagua aliazimia kumwandikia barua inspekta mkuu wa polisi Douglas Kanja kwa ajili ya kuhakikisha  kuwa matakwa  ya  kuhakikishiwa  kuwa  anapewa ulinzi katika  mikutnao yake  ya  kisiasa  linatekelezwa, Serikali kupitia  kwa usalama  wa  ndani ihakikishe kuwa familia yake inalindwa ipasavyo miongoni mwa matakwa mengine.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved