logo

NOW ON AIR

Listen in Live

DJ afariki baada ya kuzirai katika ofisi za kituo cha redio

Mcheza santuri Alex Nderi almaarufu kama DJ Lithium alifariki alipokuwa anapokea matibabu katika hospitali ya Nairobi baada ya kuzirai akiwa ofisini.

image
na

Burudani20 January 2022 - 05:06

Muhtasari


• Mcheza santuri Alex Nderi almaarufu kama DJ Lithium alifariki alipokuwa anapokea matibabu katika hospitali ya Nairobi baada ya kudaiwa kunywa sumu  kuua panya.

• Kabla ya kuchukua hatua ya kujitoa uhai DJ Lithium pia aliandikia familia na marafiki wake ujumbe akiwafahamisha kwamba ameenda.

Hofu ilitanda katika kituo kimoja cha Redio cha hapa nchini usiku wa Jumatano baada ya  mcheza santuri wao mmoja kuzirai ndani ya studio.

Mcheza santuri Alex Nderi almaarufu DJ Lithium alifariki alipokuwa anapokea matibabu katika hospitali ya Nairobi baada ya kuzirai akiwa ofisini.

Duru za kuaminika zimesema kwamba DJ Lithium aliacha kama ameandika barua. Baada ya kuona ameanguka, wafanyikazi wenzake walijitahidi kumwamsha bila mafanikio.

Wafanyakazi wenza wamesema wataachia familia ya mwenda zake  jukumu la kufungua barua ambayo marehemu aliacha. 

DJ huyo anaripotiwa kufuta kurasa zake zote za mitandao ya kijamii kabla ya kuzimia.

Polisi wameanzisha uchunguzi kuhusu tukio hilo.

Mkuu wa polisi wa Kilimani Muturi Mbogo amesema Lithium alipelekwa hospitalini kwa ambulans.

"Alithibitishwa kufariki alipofika," alisema.

Kisa hicho kilitokea katika Jumba la Lonroh katikati mwa jiji la Nairobi ingawa polisi walifahamishwa baadaye.

Kulingana na mmoja wa wafanyakazi wenzake, DJ huyo alitaja masuala ya kifamilia kuwa miongoni mwa sababu zilizomfanya achukuwe hatua hiyo.

"Alikuwa na maswala ya kifamilia ambayo alitaja kuwa sababu ya tukio hilo. Tumeshtuka,” alisema mmoja wa wafanyakazi hao.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved