logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wanafunzi 7 wakamatwa baada ya kupatikana wakitengeneza filamu za watu wazima Kakamega

Maafisa wa usalama watafuata miongozo zaidi ili kukamata washirika wengine wowote wanaohusika.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri30 October 2023 - 11:32

Muhtasari


•Walipatikana wakishiriki katika upigaji wa filamu za watu wazima ndani ya jumba la ghorofa katika Wadi ya Mwiyala, Kaunti Ndogo ya Shweye, kaunti ya Kakamega.

•Washukiwa walitiwa mbaronbi na zana zao zikiwemo kamera, kompyuta na vifaa vingine vya kielektroniki vinavyohusishwa na utayarishaji wa maudhui chafu.

 

Vijana saba wa kike walizuiliwa siku ya Jumapili na maafisa wa polisi katika kaunti ya Kakamega baada ya kudaiwa kupatikana wakijihusisha na utayarishaji wa maudhui chafu.

Washukiwa hao, ambao baadhi yao wanaaminika kuwa wanafunzi wa chuo kikuu wanaripotiwa kupatikana wakishiriki katika upigaji wa filamu za watu wazima ndani ya jumba la ghorofa katika Wadi ya Mwiyala, Kaunti Ndogo ya Shweye, kaunti ya Kakamega.

Kamanda wa polisi kaunti ya Kakamega, Joseph Kigen alithibitisha kisa hicho na kufichua kuwa washukiwa walitiwa mbaroni wakiwa na zana za kazi na vifaa mbalimbali, zikiwemo kamera, kompyuta na vifaa vingine vya kielektroniki vinavyohusishwa na utayarishaji wa maudhui chafu.

Kigen alibainisha kuwa Kurugenzi ya Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) inashughulikia suala hilo na uchunguzi umeanzishwa. Washukiwa waliwekwa chini ya ulinzi wakisubiri kuhojiwa. Vifaa vyao vilichukuliwa kwa uchunguzi wa kitaalamu ili kuthibitisha kuwa kweli walishiriki katika shughuli hizo mbaya.

Wakaazi wa Shweye walibaini kuwa washukiwa hao ambao ni pamoja na raia wa Uganda waliishi maisha ya kifahari na walitenda kwa maadili tofauti hadharani ili kuondoa tuhuma zozote za shughuli zao na majirani zao.

Wenyeji waliozungumza na vyombo vya habari walikemea vikali shughuli hiyo wakibainisha kuwa wazazi wa wanafunzi hao wanaamini kuwa watoto wao wako shuleni wakisoma. Sasa wameitaka serikali kushughulikia suala hilo kwa kina na kuchukua hatua za kuzuia kujirudia.

Maafisa wa usalama watafuata miongozo zaidi ili kukamata washirika wengine wowote wanaohusika.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved