logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Barcelona vs Real Madrid: wembe wa Messi bado una makali?

Barcelona vs Real Madrid: wembe wa Messi bado una makali?

image
na

Habari02 October 2020 - 10:13
Klabu mbili bora zaidi katika ligi ya Uhispania hii leo watakuwa wanachuana ugani Camp Nou nyumbani kwao Barcelona.

Mechi hiyo almaarufu "Elclasico" imengojewa kwa hamu na mashabiki wa soka na leo hii baada ya dakika 90 itakuwa wazi bayana klabu gani bora zaidi.

Mara ya mwisho klabu hizo kuchuana  Ernesto Valverde ambaye ni mkufunzi wa Barca alishinda mechi hiyo.

 Real Madrid wanashikilia nafasi ya pili kwa sasa wakiwa na pointi 35 nyuma yao Barcelona ambao vile vile wana pointi 35 huku wingi wa mabao ikiwatenganisha.

Barca itakuwa inategemea huduma za washambulizi Messi, Suarez, na Griezmann huku Real wakitegemea huduma za Benzema, Vinicious Junior na Toni Kroos.

Nani ataibuka mshindi? Yote hayo, yatathibitishwa leo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved