Barcelona vs Real Madrid: wembe wa Messi bado una makali?

Klabu mbili bora zaidi katika ligi ya Uhispania hii leo watakuwa wanachuana ugani Camp Nou nyumbani kwao Barcelona.

Mechi hiyo almaarufu "Elclasico" imengojewa kwa hamu na mashabiki wa soka na leo hii baada ya dakika 90 itakuwa wazi bayana klabu gani bora zaidi.

Mara ya mwisho klabu hizo kuchuana  Ernesto Valverde ambaye ni mkufunzi wa Barca alishinda mechi hiyo.

 Real Madrid wanashikilia nafasi ya pili kwa sasa wakiwa na pointi 35 nyuma yao Barcelona ambao vile vile wana pointi 35 huku wingi wa mabao ikiwatenganisha.

Barca itakuwa inategemea huduma za washambulizi Messi, Suarez, na Griezmann huku Real wakitegemea huduma za Benzema, Vinicious Junior na Toni Kroos.

Nani ataibuka mshindi? Yote hayo, yatathibitishwa leo.