logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Tutafanya Usajili wa kutosha msimu huu ukimalizika –Ole Gunnar Solkjaer asema.

Tutafanya Usajili wa kutosha msimu huu ukimalizika –Ole Gunnar Solkjaer asema.

image
na

Burudani02 October 2020 - 09:35
NA NICKSON TOSI

Meneja mkuu wa klabu ya Manchester United Ole Gunnar amesema kuwa, licha ya ligi kuu ya Uingereza kusitishwa kutokana na janga la Corona, klabu yake ya Manchester imejiandaa vyema ili kusajili wachezaji ambao wamekuwa wakiwaangazia msimu huu wote.

Akizungumza na shirika la michezo la Sky Sport, Ole amesema kuwa mikakati yote imewekwa ili kuhakikisha kuwa klabu hiyo inasajili wachezaji ambao wataifanya United kukabiliana na ushindani kutoka kwa vilabu vingine mahasidi.

Wakati uo huo, Solkjaer amesema hatua ya kusitishwa kwa ligi kuu ya Uingereza kumefanya wachezaji kama Marcus Rashford na Paul Pogba kupata nafuu baada ya kuwa nje kwa muda kutokana na majeraha ambayo walipata mwanzoni mwa msimu. Ameongeza kuwa, kurejea kwa wachezaji hao kutapiga cheki kikosi chake iwapo ligi itarejelea hali yake ya kawaida.

United wamekuwa wakihusishwa na usajili wa wachezaji Jack Grealish na Jordan Sancho


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved