logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Michezo! Wachezaji wa Arsenal wakataa kupunguza mishahara yao

Michezo! Wachezaji wa Arsenal wakataa kupunguza mishahara yao

image
na

Yanayojiri02 October 2020 - 06:20

NA NICKSON TOSI

Kikosi cha Kwanza cha Arsenal kimepusilia mbali pendekezo la Usimamizi wa klabu hiyo la kutaka kupunguziwa mshahara wao kwa asilimia 12.5 kwa muda wa mwaka mmoja kufuatia hasara waliyosajili wakati huu ambapo hakuna shughuli zozote za  ligi kuu ya Uingereza zinazoendelea.

Hatua ya kupunguza mshara wa wachezaji wa Arsenal ilionekana kama ya kupunguzia gharama uongozi wa klabu hiyo haswa wakati huu ambapo ligi takriban zote ulimwenguni zimesitishwa kutokana athari ambazo zimetokana na Corona.

 Baadhi hya wachezaji wanaolipwa mishahara nono katika klabu hiyo ya Ungereza ni Mesut Ozil anayelipwa £350,000, Pierre-Emerick Aubameyang na  Alexandre Lacazette  £200,000 .

Ligi kuu ya Uingereza ilisitishwa baada ya wachezaji na mameneja wa timu mbalimbali kupatikana na virusi vya Corona, hali iliyofanya shirikisho la soka la Uingereza FA na usimamizi wa Premier league kusitisha ligi hiyo kwa ghafla.

Aidha timu na wachezaji wamekuwa wakishauriwa na wakuu wa serikali kukubali kupunguziwa mishahara kwa asilimia 30 ili kutoa mchango kwa serikali kufanikisha shughuli za kutoa huduma kwa wananchi wa taifa hilo ambalo limeathirika pakubwa na virusi vya Corona.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved