logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mikel Kiprotich Mutai apigwa marufuku ya miaka 4 kwa kutumia dawa za kutitimua misuli

Mikel Kiprotich Mutai apigwa marufuku ya miaka 4 kwa kutumia dawa za kutitimua misuli

image
na

Yanayojiri02 October 2020 - 09:06
Doping
Jaribio la Kenya kutaka kuzuiya matumizi ya dawa za kutitimua ama kusisimua misuli na wanariadha nchini limepata pigo baada ya shirika la Athletics Integrity Unit AIU kumpiga marufuku ya miaka 4 mwanariadha wa masafa marefu Mikel Kiprotich Mutai kwa matumizi ya dawa hizo.

Yakijiri hayo pia mwanariadha mwengine Japheth Kipchir chir Kipkorir amepigwa marufuku kwa kutumia dawa zilizokuwa zimekatazwa  na shirika hilo.

AIU ilitoa taarifa hiyo ya kumpiga marufuku Mutai kupitia ukurasa wao wa Twitter .Marufuku hayo sasa yataanza kutekelezwa  kuanzia mwezi huu.

Shirika la Anti Dopping Agency la kenya ADAK na lile la riadha nchini Athletics Kenya kwa miaka miwili sasa yamekuwa yakieneza hamasisho ya kuwataka wanariadha wa humu nchini kukoma kutumia dawa hizo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved