logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Ufaransa yataka ufafanuzi zaidi wa kumalizika kwa ligi mapema

Ufaransa yataka ufafanuzi zaidi wa kumalizika kwa ligi mapema

image
na

Burudani02 October 2020 - 09:05
03fb6da73b317c42f84a390897f275d79b9ea214
Mzozo umeanza kuibuka baina ya serikali na usimamizi wa ligi kuu ya Ufaransa French League 1 baada ya wakuu wa ligi hiyo kutangaza kumalizika kwa msimu 2019/2020 zikiwa zimesalia mechi 10 kutokana na virusi vya corona ambavyo vimeathiria taifa hilo.

Hatua ya serikali ya kutaka ufafanuzi zaidi kuhusiana na hatua hiyo inajiri baada ya ligi zingine ulimwenguni kama Bundesliga,Premier League na Serie A zikipania kurejea wiki lijalo .

Uamuzi wa kusitishwa ligi kuu ya Ufaransa umetajwa kama wa kiupuzi na serikali na sasa wanataka washikadau katika ligi hiyo kufafanua ni kwa nini uamuzi uliafikiwa mapema.

“Like idiots” was the headline on the front of L’Equipe on Friday, as the sports daily questioned why such a hasty decision was made by the league (LFP) to end the season.taarifa ya serikali.

Hata hivyo wasimamizi wa ligi hiyo wamesema kuwa waliafikia kuchukuwa hatua hiyo baada ya waziri mkuu kuongezea makataa ya watu kutotangamana eneo moja ili kuzuiya maambukizi Aprili mwaka huu.

Kufikia sasa Ufaransa imesajili vifo vilivyotokana na corona takriban 29000,idadi kubwa kuliko Ujerumani japo ndogo zaidi kuliko Uingereza,Amerika ,Uhispania na Brazil.

RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved