logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Arsenal wapata kichapo kutoka kwa Burnley cha bao 1-0

Gunners walikuwa wanatarajia kutumia mechi hiyo kurejea katika mtindo wao wa ushindi

image
na Radio Jambo

Habari14 December 2020 - 06:04

Muhtasari


  • Bao la kujifunga la Pierre-Emerick Aubameyang katika awamu ya pili liliweka mwanya katika mechi ya Arsenal dhidi ya Burnley

Mechi kati ya Arsenal na Burnley ilisubiriwa sana na mashabiki huku wengi wakitabiri kwamba Arsenal wataibuka washindi katika mechi hiyo.

Bao la kujifunga la Pierre-Emerick Aubameyang katika awamu ya pili liliweka mwanya katika mechi ya Arsenal dhidi ya Burnley mnamo Jumapili, Disemba 1-0 huku mchezo huo ukitamatika 1-0.

Gunners walikuwa wanatarajia kutumia mechi hiyo kurejea katika mtindo wao wa ushindi baada ya kupokezwa kichapo cha 2-0 mechi yao ya awali dhidi ya Tottenham.

 

Hata hivyo, licha ya kutawala dakika za mapema za mechi hiyo, Arsenal walishindwa kupenyeza katika ngome ya Burnley ambao safu yao ulinzi ilibanwa vizuri.

Arsenal walikuwa na nafasi nzuri zaidi ya wazi kunako dakika ya 21 kupitia kwa Rob Holding ambaye alimalizia krosi iliyochanjwa na Saka akitumia kichwa.

Licha ya Arsenal kujikakamua na kuonekana wenye ujasiri mkubwa nguvu zao ziliambulia patupu baada ya yao kujifunga.

Mambo yaliwalemea Arsenal katika dakika ya 73 baada ya Aubameyang kuelekeza mpira kwenye lango lake kutokana na kona iliyochanjwa na Westwood.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved