Mshambulizi Lacazette amezewa mate na klabu ya Monaco

arsenal1
arsenal1

Mlinzi wa timu ya Uhispania Hector Bellerin, 25, anaweza kuondoka Arsenal msimu huu kama sehemu ya makubaliano na meneja Mikel Arteta. (ESPN)

Mlinzi wa Austria David Alaba, 28, ambaye ameiambia Bayern Munich kuwa ataondoka mwishoni mwa msimu huu, ameazimia kujiunga na klabu ambayo itamuwezesha kucheza katika safu ya kati kuliko safu ya ulinzi. Amekuwa akihusishwa na klabu ya Real Madrid, huku Chelsea, Liverpool na Manchester United pia wakimtaka. (Le Parisien, via Star)

Liverpool wanafuatilia hali ya mshambuliaji wa Real Madrid Mbrazili Rodrygo, 20, ambaye anaweza kuruhusiwa kuondoka upande wa La Liga kwa pauni milioni 50. (Diario Gol, via Team Talk)

Winga wa Arsenal Mbrazili Willian, 32, anasema alitaka kubaki katika klabu ya Chelsea lakini the Blues walikuwa wanampatia mkataba wa miaka miwili tu, badala ya miaka mitatu. (UOL Esporte, via Mail)

willian cover
willian cover

Kiungo wa kati wa Manchester City Mjerumani Ilkay Gundogan, 30, anasema Manchester United ilianza mazungumzo ya kusaini mkataba nae kuanzia Borussia Dortmund miaka miwili au mitatu kabla ya kuhamia katika City. (Sky Sports, via Mirror)

Kiungo wa kati wa Shalke, ambaye ni mchezaji wa kimataifa wa Marekani Weston McKennie ni mchezaji anayepewa kipaumbele kununuliwa na Juventus licha ya kwamba kijana huyo mwenye umri wa miaka 22-bado anakipengele cha mkataba wake cha mkopo kinachoilazimu klabu ya Tulin kumnunua . (Calciomercato - in Italian)