logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mason Mount ndiye mchezaji bora Chelsea msimu huu

Mount amepewa tuzo la mchezaji bora kwenye timu ya wanaume baada ya kuisaidia timu kufika fainali mbili.

image
na Radio Jambo

Habari20 May 2021 - 08:17

Muhtasari


Mount amepewa tuzo la mchezaji bora kwenye timu ya wanaume baada ya kuisaidia timu kufika fainali mbili.

Mason Mount

Kiungo mshambulizi wa timu ya Chelsea, Mason Mount ameshinda tunzo la mchezaji  bora katika klabu hiyo msimu huu.

Mchezaji huyo raia wa uingereza na ambaye  ana miaka 22 amelishinda tuzo hilo baada ya kusaidia klabu hiyo kufika fainali mbili ikiwemo ya kombe la FA na kombe la mabingwa Ulaya(Champions League)

Mount ameifungia klabu ya Chelsea mabao sita na kusaidia kufungwa kwa mabao tano katika kombe la EPL huku akiwa mfungaji bora wa pili katika klabu hiyo.

Huku akipokea tuzo hilo, Mount amekisifia chuo cha kufunzia kandanda cha Chelsea na kushukuru mashabiki wa timu hiyo kwa kumuunga mkono.

"Niwekea wakfu tuzo hili chuo cha kufunzia kandanda cha Chelsea na nawashukuru mashabiki wa timu hii kwa upendo mnaoendelea kunipa" Mount alisema.

Kwa sasa Chelsea imeshikilia nambari tatu ikiwa na alama 67 ikiwa nyuma ya Manchester United na Manchester City.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved