Mount amepewa tuzo la mchezaji bora kwenye timu ya wanaume baada ya kuisaidia timu kufika fainali mbili.
Kiungo mshambulizi wa timu ya Chelsea, Mason Mount ameshinda tunzo la mchezaji bora katika klabu hiyo msimu huu.
Mchezaji huyo raia wa uingereza na ambaye ana miaka 22 amelishinda tuzo hilo baada ya kusaidia klabu hiyo kufika fainali mbili ikiwemo ya kombe la FA na kombe la mabingwa Ulaya(Champions League)
Mount ameifungia klabu ya Chelsea mabao sita na kusaidia kufungwa kwa mabao tano katika kombe la EPL huku akiwa mfungaji bora wa pili katika klabu hiyo.
Men's Player of the Year. đź‘Ź pic.twitter.com/t1BhSjBxiQ
— Chelsea FC (@ChelseaFC) May 18, 2021
Huku akipokea tuzo hilo, Mount amekisifia chuo cha kufunzia kandanda cha Chelsea na kushukuru mashabiki wa timu hiyo kwa kumuunga mkono.
"Niwekea wakfu tuzo hili chuo cha kufunzia kandanda cha Chelsea na nawashukuru mashabiki wa timu hii kwa upendo mnaoendelea kunipa" Mount alisema.
I dedicate this special award to the academy, thank you for your continued support Chels fans! pic.twitter.com/82qFsrz626
— Mason Mount (@masonmount_10) May 19, 2021
Kwa sasa Chelsea imeshikilia nambari tatu ikiwa na alama 67 ikiwa nyuma ya Manchester United na Manchester City.