logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Majeruhi wa Ligi Kuu - 'Wachezaji hawawezi tena kukabiliana na mzigo huu uliokithiri'

Timu 20 za Ligi kuu za Uingereza kwa sasa zina jumla ya wachezaji 112 ambao wamejeruhiwa.

image
na SAMUEL MAINA

Michezo01 October 2023 - 05:12

Muhtasari


  • •Kocha wa Manchester City Pep Guardiola anafikiri wachezaji wanapaswa kukusanyika ili kulazimisha mabadiliko ya ratiba.

"Wachezaji hawawezi tena kukabiliana na mzigo huu."

Hayo ni maneno ya kusikitisha ya Erik ten Hag wakati meneja wa Manchester United akipambana na orodha inayoongezeka ya majeruhi.

Mholanzi huyo alikuwa akizungumza siku ambayo mlinzi wake Lisandro Martinez alitolewa nje hadi mwisho wa mwisho , na hivyo kufanya jumla ya wachezaji wasiokuwepo United kufikia wanane.

Lakini Ten Hag sio meneja pekee wa Premier League ambaye atakabiliwa na orodha ndefu ya majeruhi wiki sita tu baada ya msimu mpya.

Kocha wa Manchester City Pep Guardiola anafikiri wachezaji wanapaswa kukusanyika ili kulazimisha mabadiliko ya ratiba.

Meneja wa Newcastle Eddie Howe, meneja wa Arsenal Mikel Arteta na mkufunzi wa Chelsea Mauricio Pochettino pia wamekuwa na maoni yao kuhusu suala hilo.

Kulingana na PremierInjuries.com, Timu 20 za Ligi kuu za Uingereza kwa sasa zina jumla ya wachezaji 112 ambao wamejeruhiwa.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved