logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Haaland avunja kimya kuhusu meme yake akimfokea refa kwenye mechi dhidi ya Spurs

Alisema kwamba meme hiyo kwa mara ya kwanza ilimfanya kutabasamu mwenyewe.

image
na Davis Ojiambo

Michezo05 December 2023 - 05:42

Muhtasari


  • • Picha moja ilionyesha Haaland katika kipengele chake cha hasira, lakini ilipigwa picha kwenye kipande cha mchoro.
Erling Haaland

Fowadi wa Manchester City, Erling Haaland amevunja kimya chake kuhusu picha yake akimfokea refa wakati wa mechi yao dhidi ya Tottenham Hotspurs wikendi.

Picha hiyo imegeuzwa meme na wengi wamekuwa wakiieneza kwa jinsi ambavyo raia huyo wa Norway alikuwa amafoka kwa hasira dhidi ya muamuzi wa mechi hiyo iliyoishia sare ya mabao 3-3.

Mambo yangeenda tofauti kama mwamuzi Simon Hooper alicheza kwa faida katika dakika za kufa wakati Grealish alifunga bao.

Hooper alipuliza kipenga cha kumfanyia madhambi Haaland, na kumaliza shambulizi hilo na kumwacha mshambuliaji na wachezaji wengine wa Manchester City wakiwa wamekasirishwa na uamuzi huo.

Halaand aliadhibiwa kwa maandamano yake, lakini huo haukuwa mwisho kwani aliendelea kumzomea mwamuzi baada ya kipyenga cha muda wote.

Kama ilivyoripotiwa na BBC, Haaland baadaye alishiriki hisia zake kwenye mitandao ya kijamii, akichapisha picha za tukio hilo pamoja na maelezo mafupi.

Uamuzi wa utata wa Simon Hooper unaweza kuwa ndio mazungumzo ya kwanza baada ya mchezo. Hata hivyo, hiyo ilibadilika Jumatatu, Desemba 4 huku watumiaji wa mtandaoni wajanja walipoona upande wa kuchekesha wa kejeli za Haaland, Sports Brief walibaini.

Meme ya Haaland tangu wakati huo yamekuwa yakisumbua mitandao ya kijamii, na mshambulizi huyo wa zamani wa Borussia Dortmund alifurahishwa na baadhi ya picha za ubunifu zinazosambazwa mtandaoni.

Picha moja ilionyesha Haaland katika kipengele chake cha hasira, lakini ilipigwa picha kwenye kipande cha mchoro.

Alisema kwamba meme hiyo kwa mara ya kwanza ilimfanya kutabasamu mwenyewe.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved