logo

NOW ON AIR

Listen in Live

AFCON 2023: Tazama matokeo ya Jumanne, Ratiba ya michuano ya Jumatano

Afrika Kusini ilipata kichapo kibaya cha mabao 2-0 dhidi ya Mali huku mabao yote mawili yakifungwa katika kipindi cha pili.

image
na SAMUEL MAINA

Michezo17 January 2024 - 06:03

Muhtasari


  • •Mashindano ya AFCON 2023 yaliingia siku ya nne mnamo Jumanne, Januari 16, huku mechi tatu zikichezwa jioni.
  • •Afrika Kusini ilipata kichapo kibaya cha mabao 2-0 dhidi ya Mali huku mabao yote mawili yakifungwa katika kipindi cha pili.
ilipata ushindi wa 2-0 dhidi ya Afrika Kusini

Mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON 2023) yanayoendelea nchini Ivory Coast yaliingia siku ya nne mnamo Jumanne, Januari 16, huku mechi tatu zikichezwa jioni

Mechi ya kwanza kati ya Burkina Faso na Mauritania ilishuhudia timu hizo mbili ambazo zilionekana kuwa na nguvu sawa zikichuana vikali hadi kukaribia kumaliza mchuano huo kwa sare kabla ya mshambuliaji wa Aston Villa Bertrand Traore kuifungia Burkina Faso bao la ushindi katika dakika ya 90+6. 

Timu zote mbili zilikuwa zimekosa nafasi nyingi za kufunga katika mechi yote lakini Mauritania ilivunjwa moyo katika dakika za mwisho na kuwaachwa katika nafasi ya mwisho katika kundi D.

Namibia pia walipata ushindi wa kushtukiza wa 1-0 dhidi ya moja ya miamba ya soka wa Afrika Kaskazini, Tunisia baada ya kuonyesha mchezo mzuri katika mechi hiyo iliyochezwa saa mbili jioni.

Mshambulizi wa Orlando Pirates, Deon Hotto aliifungia Namibia bao la ushindi katika dakika ya 88 baada ya nchi hiyo ya Afrika Kusini kuwapa wakati mgumu wapinzani wao katika muda wote wa mechi.

Afrika Kusini ilipata kichapo kibaya cha mabao 2-0 dhidi ya Mali huku mabao yote mawili yakifungwa katika kipindi cha pili.

Mchezaji wa zamani wa Brighton, Percy Tau alikosa penalti katika kipindi cha kwanza kabla ya Hamari Traore na Lassine Sinayoko kuifungia Mali mabao mawili katika dakika ya 60 na 66 mfululizo.

Mashindano hayo sasa yanaingia siku ya tano mnamo Jumatano, Januari 16 huku mechi mbili pekee zikichezwa jioni.

Tazama ratiba ya mechi za Jumatano hapa chini;-

KUNDI F: Morocco vs Tanzania (Saa mbili usiku masaa ya Afrika Mashariki, katika uwanja wa Stade Laurent Pokou (San Pedro)

Kundi F: D.R Congo (Saa tano usiku masaa ya Afrika Mashariki, katika uwanja wa Stade Laurent Pokou (San Pedro)


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved