logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Bundesliga yapata nafasi ya ziada katika ligi ya mabingwa 2024/25

Timu za Bundesliga za pata nafasi ya ziada kwa 2024/25.

image
na Davis Ojiambo

Michezo02 May 2024 - 07:56

Muhtasari


  • •Timu nne zinazowania kubeba ubigwa wa Ulaya.
  • •Timu za Bundesliga zinapata nafasi ya ziada kwa 2024/25.

Nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya  hatua ya kwanza ilianza kwa  kufurahisha na mchezo wa kusisimua. Kwa siku mbili zilizopita, ulimwengu wa soka ulishuhudia mapambano kati ya timu nne zinazowania kubeba ubigwa wa Ulaya.

Nusu fainali ya kwanza ilishuhudia makabiliano kati ya mabingwa mara kwa mara Bayern Munich wa Ujerumani na  Real Madrid kutoka Uhispania.

Timu zote mbili zilikua na mchezo mzuri. Bayern Munich, wakiongozwa na hamu yao ya kulinda ubingwa wao, walituma mashambulizi yasio na mwisho, wakijaribu kuzimi azimio ya Real Madrid kutamba kwenye pambano hilo.

Pambano hilo iliisha sare ya mabao mawili, wiki ijawayo Real Madrid watakuwa wenyeji wa Bayern Munich katika hatua ya pili ambapo kila timu itakua na hamu ya kuingia fainali.

Pambano lingine ilishuhudia Borussia Dortmund kutoka Ujerumani ilikutana na Paris Saint-Germain ya Ufaransa.

 Timu zote mbili zilionyesha ustadi wao wa kushambulia na azimio lao la kufika fainali. Borussia Dortmund, walitumia uwanja wao wa  nyumbani na kuonyesha mchezo mzuri na baada ya kipenga cha mwisho walikua washindi.

Pambano hizo zitarejelewa kwa mara ya  pili wiki ijayo na kila timu itakua inawania kufika fainali na kubeba taji hilo la Mabigwa Ulaya.

Ushindi wa Borussia Dortmund dhidi ya PSG usiku wa kuamkia leo umefanya  Ligi ya Italia kuwakilishwa na  timu tano katika  michezo wa Mabingwa Ulaya msimu ujao na ina maana kwamba ni timu nne tu bora za Ligi Kuu ya Uingereza zitafuzu.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved