logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Chelsea yamteua Maresca kama kocha mpya

Maresca, 44, alichukua jukumu la kuinoa Foxes mnamo Juni 2023 na kuwaongoza kuchukua ubingwa msimu uliopita

image
na Samuel Maina

Michezo04 June 2024 - 04:15

Muhtasari


  • •Muitaliano huyo anachukua nafasi ya Mauricio Pochettino, ambaye aliondoka kwa makubaliano tarehe 21 Mei baada ya msimu mmoja tu Stamford Bridge.

Chelsea wamemteua mkufunzi wa Leicester Enzo Maresca kama kocha wao mpya kwa kandarasi ya miaka mitano na chaguo la nyongeza ya mwaka.

Muitaliano huyo anachukua nafasi ya Mauricio Pochettino, ambaye aliondoka kwa makubaliano tarehe 21 Mei baada ya msimu mmoja tu Stamford Bridge.

Maresca, 44, alichukua jukumu la kuinoa Foxes mnamo Juni 2023 na kuwaongoza kuchukua ubingwa msimu uliopita

"Kujiunga na Chelsea, moja ya klabu kubwa duniani, ni ndoto kwa kocha yeyote," alisema. "Ndio maana nimefurahishwa sana na fursa hii.

"Ninatarajia kufanya kazi na kundi la wachezaji na wafanyikazi wenye vipaji ili kukuza timu ambayo inaendeleza utamaduni wa mafanikio wa klabu na kuwafanya mashabiki wetu wajivunie."

Maresca, ambaye ataanza kazi yake mpya Julai 1, ni kocha wa Chelsea katika kipindi cha miaka mitano na wa nne tangu mwekezaji Mmarekani Todd Boehly na kampuni ya hisa ya Clearlake Capital kuinunua klabu hiyo Mei 2022.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved