Droo ya hatua ya kumi na sita bora kwenye mashindano ya kombe la bara Ulaya ,Euro 2024 imekamilika baada ya mechi za makundi kufikia mwisho Juni 26.
Timu zilizomaliza nafasi ya kwanza na ya pili kwenye hatua ya makundi zimejikatia tiketi huku timu nne zikiongezwa zilizomaliza katika nafasi ya tatu almaarufu kama 'best losers'.
Kikosi cha Gareth Southgate kitamenyana na Slovania baada ya kumaliza nafasi ya kwanza kwenye kundi lao Jumapili 30.
Mabingwa watetezi Italy watakuwa na kibarua dhidi ya Switzerland waliomaliza kwenye nafasi ya pili,kundi A nyuma ya Ujerumani,ambao sasa wapo mawindoni kwa taji hilo wakiwa wenyeji wa michuano hio na watatifuana na Denmark
Hatimaye ushindi wa Georgia wa 2-0 dhidi ya Ureno usiku wa Jumatano ulliwakikishia kufuzu kwenye hatua ya kumi na sita bora baada ya kumaliza wa pili kwenye kundi F na watakwaruzana dhidi ya Uhsipania.
Romania watacheza na Uholanzi katika mechi yao ya kwanza ya mtoano ya mashindano kwa miaka 24 huku kikosi cha aliyekuwa meneja wa Manchester United ,Ralf Rangick Autria kikimaliza udhia dhidi ya Uturiki.
Mechi inayotazamiwa kuwa na mvuto zaidi itawahusisha mabingwa wa kombe la dunia wa mwaka 2018 ,Ufaransa watakapotoana kivumbi dhidi ya Ubelgiji.
Hii hapa ni droo kamili:
Italy vs Switzerland
Germany vs Denmark
England vs Slovakia
Spain vs Georgia
France vs Belgium
Portugal vs Slovenia
Romania vs Netherlands
Austria vs Turkey
Mechi hizo za hatua ya kumi na sita bora zinatazamiwa kuanza Jumamosi ,Juni 29 hadi Julai 2,2024.