logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Euro 2024: Uhispania na England zatinga robo fainali

Uhispania walitinga hatua ya robo fainali na wenyeji Ujerumani kwa kunusurika na hofu ya mapema ya kuondolewa na Georgia.

image
na SAMUEL MAINA

Michezo01 July 2024 - 04:07

Muhtasari


  • •Uhispania walitinga hatua ya robo fainali na wenyeji Ujerumani kwa kunusurika na hofu ya mapema ya kuondolewa na Georgia.

Uhispania walitinga hatua ya robo fainali na wenyeji wa michuano ya Euro 2024 Ujerumani kwa kunusurika na hofu ya mapema ya kuondolewa na Georgia baada ya kwa kupata ushindi wa maao 4-1.

Wakicheza katika mchuano wao wa kwanza muhimu, Georgia ililazimika kupata presha kubwa kutoka kwa Uhispania mapema lakini ikawashangaza wengi katika Uwanja wa Cologne walipopata uongozi wa kushtukiza baada ya dakika 18.

Beki wa Uhispania Robin le Normand alichombeza krosi ya Otar Kakabadze kwenye lango lake, akimalizia shambulizi la kushtukiza na kuwanyamazisha mashabiki nyuma ya lango lao.

Wachezaji wa akiba waliokuwa wakipasha misuli motowalimkimbilia Khvicha Kvaratskhelia, ambaye aliongoza sherehe za Georgia kwenye kona.

Jude Bellingham alionyesha kipaji cha kipekee baada ya kuiokoa England kwa kuwabakiza katika katika Euro 2024 baada ya hofu ya kuyaaga mashindano hayo alipofunga bao ambalo liliwapa ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Slovakia kwa mtindo wa ajabu na kutinga hatua ya nane bora.

England walikuwa wamesalia sekunde chache kuyaaga mashindano hayo huku Slovakia wakilinda bao lao la kuongoza ambalo walikuwa wameshikilia tangu dakika ya 25 pale Ivan Schranz alipoingia kwenye eneo la hatari na kumshinda kipa wa Uingereza Jordan Pickford.

Hapo ndipo Bellingham, ambaye alisherehekea siku yake ya kuzaliwa ya mwaka wa 21 siku ya Jumamosi, alionyesha umahiri wake ambao umemfanya kuwa supastaa mpya wa England kwa kupaa angani katika eneo la hatari kuusuka vyema mpira wa kichwa wa Marc Guehi kumpita Martin Dubravka kwa kiki ya ajabu 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved