logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Messi:Si rahisi kuwa kwenye fainali nyingine

Argentina itachuana na mshindi kati ya Canada na Uruguay kwenye fainali ya Copa America.

image
na Davis Ojiambo

Michezo10 July 2024 - 07:05

Muhtasari


  • •Lionel Messi alifunga kwenye nusu fainali kati ya Argentina na Canada na kuiwezesha Argentina kuicharaza Canada 2-0.
  • •Nusu  fainali ya pili itawahusisha Uruguay na Colombia ,Julai 11  mwendo wa saa tisa asubuhi saa za Afrika Mashariki

Nahodha wa Argentina,Lionel Messi ameelezea furaha yake baada ya timu yake kufika kwenye fainali ya kombe la Copa America 2024 baada ya kuiadhibu Canada 2-0. 

Messi alifunga bao lake la kwanza la michuano hiyo katika dakika ya 51 na kuisaidia Argentina kuwa na bao la pili baada ya Julian Alvarez kupachika la kwanza. Kufuatia ushindi huo, Messi mwenye furaha alisema anafurahia ‘vita vyake vya mwisho’ na taifa hilo la Argentina.

“Si rahisi kuwa kwenye fainali nyingine, kushindana tena ili kuwa mabingwa, tunachokipata ni kigumu sana na tunatakiwa kutumia fursa hiyo. Si rahisi kufanya hivi na tunafanya tena," Messi alisema.

Alipoulizwa kuhusu mustakabali wake , alisema kuwa;

Ninajua, kama ilivyo kwa Otamendi, Di María na mimi, kwamba hizi ni vita vya mwisho na tunavifurahia kwa ukamilifu.”

Ushindi huo wa Argentina umewapa fursa nyingine ya kuhakikisha kuwa  wanatetea taji hilo la Copa America baada ya kuishinda  Brazil  1-0 mwaka wa 2021.

Argentina sasa itashiriki katika mpambano wa kilele huko Miami Jumapili ambapo watamenyana na mshindi kati ya  Colombia na Uruguay mechi ambayo imeratibiwa kuchezwa Alhamisi,Julai 11 2024.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved