logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Benzema Ataja Uvumi Wa Yeye Kustaafu Mwishoni Mwa Msimu Kama “Ujinga Mtupu!”

“Huku kandarasi ya Mfaransa huyo ikikamilika 2026, Benzema amekuwa akifikiria juu ya mustakabali wake,” chanzo kimoja kiliripoti.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Michezo11 January 2025 - 09:30

Muhtasari


  • Mwezi Desemba mwaka uliopita, majarida mbalimbali ya soka Ulaya yalifichua kwamba mshambuliaji huyo wa zamani wa Real Madrid alikuwa anafikiria kustaafu mwishoni mwa msimu huu.
  • “Huku kandarasi ya Mfaransa huyo ikikamilika 2026, Benzema amekuwa akifikiria juu ya mustakabali wake,” chanzo kimoja kiliripoti.



MSHAMBULIAJI wa Al-Ittihad, Mfaransa Karim Benzema amekanusha uvumi ulioripotiwa Desemba mwaka jana kwamba anafikiria kustaafu kutoka soka la kulipwa mwishoni mwa msimu huu.


Benzema ambaye amezungumzia uvumi huo kwa mara ya kwanza, ametaja tetesi hizo kama ujinga mtupu, akisisitiza kwamba mwili wake bado upo ngangari kinoma kuendelea kucheza.


“Kutastaafu baada ya msimu huu? HAPANA. SI KWELI. Upuuzi mtupu huo, nani kasema. Najisikia vizuri!", alisema Karim Benzema.


Mwezi Desemba mwaka uliopita, majarida mbalimbali ya soka Ulaya yalifichua kwamba mshambuliaji huyo wa zamani wa Real Madrid alikuwa anafikiria kustaafu mwishoni mwa msimu huu.


Benzema alitatizika katika msimu wake wa kwanza kwenye Ligi Kuu ya Saudia chini ya Nuno Espirito Santo baada ya kuondoka Real Madrid, hata hivyo, mshindi huyo wa Ballon d'Or 2022 amepata mafanikio msimu huu huku Al-Ittihad wakiongoza msimamo wa ligi dhidi ya Al-Hilal na Al- Qadsiah.


“Huku kandarasi ya Mfaransa huyo ikikamilika 2026, Benzema amekuwa akifikiria juu ya mustakabali wake,” chanzo kimoja kiliripoti.


Kulingana na ripoti hiyo, Al-Ittihad wanatarajia Benzema kutimiza mkataba wake lakini klabu hiyo haitajali iwapo mshambuliaji huyo wa Ufaransa ataondoka 2025 kwa sababu mshahara wake wa karibu Euro milioni 100 (£82.9m/$104.9m) ungewapunguzia kiasi kikubwa cha pesa. mzigo wa kifedha.


Kulingana na ripoti ya Relevo, klabu ya zamani ya Benzema, Real Madrid, ilikuwa imejipanga kuwa balozi wa klabu hiyo Mashariki ya Kati, kutokana na mahusiano ambayo mshambuliaji huyo amejenga kwa miaka mingi katika eneo hilo.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved