logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Bingwa wa kurusha mkuki Julius Yego abanduliwa nje ya mashindano ya Olimpiki yanayoendelea Tokyo

Yego alimaliza katika nafasi ya 24 baada yake kurusha mkuki umbali wa mita 77.34 chini ya alama iliyohitajika ya umbali wa 83.50.

image
na Radio Jambo

Habari04 August 2021 - 04:29

Muhtasari


•Ndoto za bingwa wa kutupa mkuki Julius Yego kuongeza medali nyingine kwenye kabati lake zilififia mapema asubuhi ya Jumatano baada yake kushindwa kufikisha alama zilizohitajika kuhitimu kuingia fainali.

•Yego ambaye alijinyakulia fedha kwenye mashindano ya Olimpiki yaliyofanyika Rio De Janeiro, Brazil mwaka wa 2016 amekuwa na msimumbaya  uliosheheniwa na majeraha.

Mwanariadha Julius Yego

Nchi ya Kenya imeendelea kupokea matokeo hafifu kwenye mashindano ya Olimpiki yanayoendelea jijini Tokyo Japan huku mabingwa waliotiliwa imani kubwa wakionekana kulemewa.

Ndoto za bingwa wa kutupa mkuki Julius Yego kuongeza medali nyingine kwenye kabati lake zilififia mapema asubuhi ya Jumatano baada yake kushindwa kufikisha alama zilizohitajika kuhitimu kuingia fainali.

Yego almaarufu kama 'YouTube Man' alimaliza katika nafasi ya 24 baada yake kurusha mkuki umbali wa mita 77.34 chini ya alama iliyohitajika ya umbali wa 83.50.

Hata hivyo, alama alizoandikisha  mwanariadha huyo katika uwanja wa Olimpiki mida ya saa kumi unusu asubuhi ndizo alama zake  bora msimu huu.

Yego ambaye alijinyakulia fedha kwenye mashindano ya Olimpiki yaliyofanyika Rio De Janeiro, Brazil mwaka wa 2016 amekuwa na msimumbaya  uliosheheniwa na majeraha.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved