logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mwanariadha wa Kenya na bingwa wa mbio za nyika mwaka 2015 Agnes Tirop ameaga dunia

Alimaliza wa nne mnamo 14: 39.62 katika mbio za mita 5,000 za wanawake

image
na Radio Jambo

Burudani13 October 2021 - 10:52

Muhtasari


  • Mwanariadha wa Kenya na bingwa wa mbio za nyika mwaka 2015 Agnes Tirop ameaga dunia

Mwanariadha wa Kenya na bingwa wa mbio za nyika mwaka 2015 Agnes Tirop ameaga dunia.

Agnes ambaye aliiwakilisha Kenya katika #tokyoolympics alipatikana na majeraha ya kuchomwa na kisu kwenye tumbo nyumbani kwake Iten, kaunti ya Elgeyo Marakwet.

Mazingira ya kifo chake bado hayajafahamika, Mwanariadha huyo nyota alikuwa ameshikilia rekodi ya dunia mwezi uliopita baada ya kushinda mbio za kilomita 10 baada ya kutumia saa 30:01 wakati wa hafla ya Adizero huko Herzogenaurach, Ujerumani.

Alimaliza wa nne mnamo 14: 39.62 katika mbio za mita 5,000 za wanawake, mbio zilizoshindwa na Mholanzi Sifan Hassan.

Polisi wameanzisha uchunguzi wa kifo chake.

Mengi yafuata;

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved