logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Omanyala avunja rekodi ya mita 60 kwa mara ya 3 nchini Ufaransa

Omanyala avunja rekodi tena kwa mara ya tatu mfululizo katika mbio huko France.

image
na Radio Jambo

Habari18 February 2022 - 09:36

Muhtasari


• Ferdinand Omanyala ameandikisha rekodi mpya katika mbio za mita 60 kwa mara ya tatu mtawalia katika mbio zilizoandaliwa Ufaransa, Februari 17

Ferdinand Omanyala

Mwanariadha Ferdinand Omanyala kwa mara nyingine tena amepeperusha bendera ya Kenya kwa madoido mno baada ya kuvunja rekodi ya mita sitini kwa mara ya tatu sasa katika mbio zilizoandaliwa nchini Ufaransa, Februari 17.

Omanyala ambaye kwa sasa anashikilia rekodi ya kuwa mwanamme mwenye mbio Zaidi barani Afrika kwa mara nyingine tena alipunguza rekodi ya kitaifa katika mbio za mita 60 kwa mara ya tatu mtawalia kwenye mashindano yaliyoandaliwa Assembly Hauts-de-France Pas-de-Calais huko Lievin nchini Ufaransa.

Katika mbio hizo, Omanyala aliandikisha rekodi ya sekunde sita nukta tano saba (6.57) na kumaliza wa nne nyuma ya Muitaliano Jacobs Marcell aliyeshinda mbio hizo kwa sekunde 6.50 akifuatiwa na Mmarekani Cravont Charleston (6.52) katika nafasi ya pili na mwenzake Elijah Corridor (6.57) kutokea Marekani pia akawa wa tatu mbele ya Omanyala.

Hii ni mara ya tatu ambapo Omanyala, 26, aliandikisha rekodi mpya kwenye mbio hizo baada ya kufanya hivo Februari 4, miezi michache tu baada ya kuvunja rekodi iliyokuwa imewekwa miaka 17 iliyopita.

Hongera sana Omanyala!


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved