logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Ethiopia yatuma salamu za rambirambi baada ya mwanariadha wa Kenya kuuawa

Polisi wanasema mwili wa Mutua ulipatikana "ukiwa katika hali mbaya " huko Iten.

image
na Radio Jambo

Habari22 April 2022 - 03:24

Muhtasari


• Polisi wanasema kuwa mpenzi wake kutoka Ethiopia, aliyetajwa kwa jina la Eskinder Hailemaryam, ni mshukiwa mkuu na anatafutwa.

Shirikisho la riadha nchini Ethiopia limetuma salamu za rambirambi kwa familia na marafiki wa mwanariadha wa Kenya Damaris Muthee Mutua, 28, baada ya kukutwa amefariki akiwa na majeraha ya kuchomwa kisu katika mji wa Iten nchini , maarufu kwa kituo chake cha wakimbiaji wa mbio ndefu.

Polisi wanasema kuwa mpenzi wake kutoka Ethiopia, aliyetajwa kwa jina la Eskinder Hailemaryam, ni mshukiwa mkuu na anatafutwa. Bado hajatoa maoni yake na inasemekana alitoroka Kenya.

Shirikisho la Riadha la Ethiopia lilimtaja Mutua kama ‘’mwanariadha shujaa’’.

Alizaliwa nchini Kenya lakini ameshindania Bahrain.

Polisi wanasema mwili wa Mutua ulipatikana "ukiwa katika hali mbaya " huko Iten.

Yeye ni mwanariadha wa pili wa kike kuuawa katika mji huo katika mwaka mmoja.

Mwaka jana, Wakenya walishangazwa na mauaji ya mwanariadha wa Olimpiki Agnes Tirop.

Mumewe bado yuko kizuizini na anakanusha mauaji.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved