logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Ulijitahidi-Mkewe Omanyala ampongeza baada ya ushindi wa Mauritius

Kulingana na mama wa mtoto mmoja, mpenzi wake alikuwa amejitahidi sana kustahili medali ya dhahabu.

image
na Radio Jambo

Habari09 June 2022 - 14:09

Muhtasari


  • Kulingana na mama wa mtoto mmoja, mpenzi wake alikuwa amejitahidi sana kustahili medali ya dhahabu
Ferdinand Omanyala

Lavender Omanyala, mke wa nyota anayechipukia kwa kasi Mkenya Ferdinand Omanyala hii leo ameelezea furaha yake baada ya ushindi wa mumewe katika Riadha za Kiafrika zilizoandaliwa Reduit, Mauritius.

Omanyala alifanikiwa kuondoka na medali ya dhahabu baada ya kuwabwaga wapinzani wake wote katika mbio za mita 100.

Omanyala inasemekana alitumia sekunde 9.927 kuwashinda wapinzani wengine wote akiwemo Ankani Simbine wa Afrika Kusini aliyeibuka wa pili.

Akiwa amefurahishwa na matokeo hayo, Lavender alitumia ukurasa wake wa Instagram huku akimmwagia sifa mchumba wake Ferdinand Omanyala.

Kulingana na mama wa mtoto mmoja, mpenzi wake alikuwa amejitahidi sana kustahili medali ya dhahabu.

"Ulijitahidi sana kuleta medali nyumbani...najivunia wewe. Utukufu, utukufu kwa Mwenyezi. Tazama mshindi wa medali ya dhahabu ya Ubingwa wa Wakubwa wa Afrika 2022,"Aliandika.

Sawa, uungwaji mkono wa Lavender kuelekea taaluma ya mumewe mara nyingi umekuwa mwingi sana.

Katika mahojiano ya awali katika kipindi cha Jeff Koinange Live, Ferdinand Omanyala hata alifichua kuwa mke aliwahi kumfadhili kifedha wakati fulani ambapo mambo bado hayakuwa sawa kwake.

Kutoka kwetu wanajambo Hongera Ferdinand Omanyala kwa mafanikio yako mapya.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved