logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wa kuvunja rekodi ya dunia ni mimi- Omanyala asema huku akijiandaa kwa fainali Mauritius

Omanyala anashikilia rekodi ya Afrika katika mbio za mita 100 (9.77).

image
na Radio Jambo

Yanayojiri09 June 2022 - 04:47

Muhtasari


•Omanyala alifuzu fainali ya Senior Africa Athletics Championships baada ya kuandikisha muda bora zaidi katika nusu fainali za kombe hilo. 

•Omanyala ameweka wazi kuwa lengo lake kuu ni kuvunja rekodi ya dunia ambayo kwa sasa inashikiliwa na Usian Bolt wa Jamaica.

Ferdinand Omanyala

Mwanariadha wa mbio za mita 100 Ferdinand Omanyala ameshikilia kuwa mawazo yake yote kwa sasa yapo kwenye fainali za Senior Africa Athletics Championships zitakazofanyika leo  (Juni 9)  jijini Reduit, Mauritius.

Omanyala ambaye ndiye anashikilia rekodi ya Kiafrika katika mbio za mita 100 alifuzu fainali ya Senior Africa Athletics Championships baada ya kuandikisha muda bora zaidi katika nusu fainali za kombe hilo. 

Mwanariadha huyo mwenye umri wa miaka 26 alikimbia kwa sekunde 10.07 huku Maseko Gilbert wa Namibia akiibuka wa pili kwa sekunde 10.15 na Noa Bibi wa Mauritius akiandikisha sekunde 10.24.

"Zilikuwa mbio nzuri...10.07 ni muda mzuri sana. Kwa hiyo sasa mawazo yangu yapo kwenye fainali, kwenye mstari wa mwisho kwa sababu unapoweka akili yako kwa washindani, utaishia kukimbia mbio zao," Omanyala alisema baada ya kufuzu kushiriki fainali.

Omanyala ameweka wazi kuwa lengo lake kuu ni kuvunja rekodi ya dunia ambayo kwa sasa inashikiliwa na Usian Bolt wa Jamaica.

Alivunja rekodi ya Afrika mwezi Septemba mwaka jana baada ya kumaliza mbio hizo kwa sekunde 9.77 wakati wa  Kip Keino Classic Tour .

"Rekodi ya dunia sio ya kipekee na hakuna lisilowezekana katika ulimwengu huu. Naamini itavunjwa na wa kuivunja ni mimi maana hakuna aliyeamini kuwa Mkenya anaweza kukimbia haraka," Omanyala alisema katika mahojiano na BBC.

Mwanariadha huyo alisema kuwa hakuwahi kufikiria angefikia hatua ambayo ameweza kufikia sasa.

Rekodi ya sasa ya dunia katika mbio za 100 ni sekunde 9.58 ambayo iliandikishwa na Usian Bolt katika mbio za IAAF World Championship mwaka wa 2009.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved