logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Chepngetich awashukuru mashabiki kwa kumtia moyo

Chepngetich aliahidi kuvunja rekodi katika mbio zake zijazo.

image
na

Habari11 October 2022 - 05:33

Muhtasari


Chepngetich alifanikiwa kutetea taji lake katika kinyang'anyiro hicho baada ya kuvunja mkanda katika muda wa saa 2, dakika 14 na sekunde 18.

Chepngetich amewashukuru mashabiki wake kwa pongezi zao kufuatia ushindi.

Ruth Chepng'etich

Bingwa wa mbio za Chicago Marathon Ruth Chepngetich amewashukuru mashabiki wake kwa pongezi zao kufuatia ushindi wake siku ya Jumapili.

Chepngetich alifanikiwa kutetea taji lake katika kinyang'anyiro hicho baada ya kuvunja mkanda katika muda wa saa 2, dakika 14 na sekunde 18.

“Nina furaha sana kwa matokeo bora siku ya Jumapili katika Benki ya Amerika ya Chicago Marathon, mbio ambazo nitazikumbuka daima! Asanteni nyote kwa ujumbe wenu mzuri. Nitachukua muda wangu kufurahia, kisha nirudi kazini. Mungu awabariki ninyi nyote,” Chepngetich alisema.

Chepngetich aliahidi kuvunja rekodi katika mbio zake zijazo.

"Nilitaka kuvunja rekodi ya dunia. Mwaka ujao niko tayari kurejea tena,” Chepngetich alisema.

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved