Drake ashinda milioni 361 kwenye kamari ya ndondi baada ya kubet kwa milioni 66 pekee!

Katika pambano la awali, Drake alibashiri Adesanya kushinda lakini bet yake ya dola milioni 1.6 ilikunywa maji baada ya Pereira kumchachafya Adesanya.

Muhtasari

• Drake aliweka dau la $500,000 kwa Adesanya na kushinda ambalo lilirejesha $885,000 na dau la $400,000 ili ashinde kwa mtoano, ambalo lilirejesha dola milioni 1.8.

Drake ashinda milioni 361 kwenye kamari ya ndondi.
Drake ashinda milioni 361 kwenye kamari ya ndondi.
Image: Insatgram

Rapa Drake alishinda $2.7million sawa na shilingi milioni 361 za Kenya baada ya Israel Adesanya kumtoa Alex Pereira kwenye mchezo wa ngumi waUFC 287 na kutwaa tena taji la uzani wa kati.

Adesanya alishinda tena taji la pauni 185 miezi mitano tu baada ya kupoteza kwa mpinzani wake mkali Pereira, ambaye hapo awali alimshinda mara mbili katika mchezo wa ndondi.

 Drake alipoteza dola milioni 1.6 baada ya kumuunga mkono Adesanya kushinda katika pambano hilo lakini alimfanyia marekebisho rapper huyo katika mechi yake ya marudiano na Pereira.

Drake aliweka dau la $500,000 kwa Adesanya na kushinda ambalo lilirejesha $885,000 na dau la $400,000 ili ashinde kwa mtoano, ambalo lilirejesha dola milioni 1.8.

Adesanya aliulizwa kuhusu dau la Drake baada ya pambano lake, ambapo alisema: "Shukrani kwa kila mmoja ambaye alinibashiria kushinda, na najua nikiingia kwenye octagon huwa naweka maisha yangu kwenye mstari. Huo ndio ushindi mkubwa kwako ninaweza kufanya. Mimi ni mtu wa kamari pia kwa hivyo ninapiga kelele, tunakaribia kufanya mpango mwingine na kupata pesa zaidi."

Drake alipata sifa mbaya kwa kamari zake za UFC alipomuunga mkono Masvidal kumpiga Colby Covington katika pambano lao la kinyongo Machi mwaka jana, lakini rapper huyo alipoteza $275,000 kwenye pambano hilo.

Bahati mbaya yake iliendelea miezi michache baadaye pale Justin Gaethje alipokabwa nje na Charles Oliveira katika pambano lao la kuwania taji la lightweight, huku hasara ya Gaethje ikimgharimu Drake $400,000.