logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mandonga Mtu Kazi na Wanyonyi kuzichapa tena mwezi Julai

Mandonga alimshinda Wanyonyi walipokutana kwa mara ya kwanza Januari 14, mwaka huu

image
na Radio Jambo

Habari21 May 2023 - 04:50

Muhtasari


•Ijumaa walibadilishana maneno ya kukosoana kama ilivyo kwa wapinzani kabla ya mechi yao ya marudiano iliyokuwa ikitarajiwa kufanyika jijini Nairobi.

Baada ya pambano la kufana la kwanza miezi minne iliyopita, sasa wanasema usubiri kwa ghamu pambano la marudiano la uzito wa juu la “Mandonga na Wanyonyi 2” ambalo linaahidi kutingisha Kituo cha Maonyesho cha Sarit Julai 22, mwaka huu, kulingana na gazeti la Daily Nation.

Mwanandondi wa Tanzania, Karim maarufu kama “Mtu Kazi” Mandonga, ambaye ni bingwa wa Pugilistic Syndicate of Tanzania (PST), na Daniel Wanyonyi, bingwa wa zamani wa taji la Afica Boxing Union (ABU) Kenya, Ijumaa walibadilishana maneno ya kukosoana kama ilivyo kwa wapinzani kabla ya mechi yao ya marudiano iliyokuwa ikitarajiwa kufanyika jijini Nairobi.

Afisa mkuu mtendaji wa kusimamia mashindano wa Ultra Fight Series Maurice Odera alifichua Ijumaa kuwa Mandonga na Wanyonyi wametia saini mkataba wa kukutana tena kwenye mchuano wa "Marudio au Kulipiza kisasi"

Mandonga alimshinda Wanyonyi walipokutana kwa mara ya kwanza Januari 14, mwaka huu katika ukumbi wa KICC.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved