Kocha wa Liverpool, Arse Slot amesema kwamba timu ya Arsenal
ni mpinzani mkuu wa Liverpool, na ni lazima vijana wake wahakikishe wanachukua alama zote tatu katika mchuano wa Jumapili.
Akizungumza kabla ya mechi hiyo inayosubiriwa Zaidi na
mashabiki wa soka duniani, kocha Slot amesema kwamba kupata alama tatu kutoka
kwa mpinzani ni muhimu kwa kuwa haijulikani ni timu gani itakuwa mpinzani mkuu
katika mechi za mwishi mwisho wa msimu.
Slot amesema kwamba anaamini kuwa timu ya Arsenal itakuwa
mpinzani mkuu wa Liverpool katika kinyang’anyiro cha kutwaa kombe la ligi kuu
Uingereza hivyo kitu cha msingi zaidi nu kupata alama wala si kupoteza.
“Katika hatua hizi za mwanzo mwanzo, hakuna anyejua ni nani atakuwa
mpinzani mkubwa, lakini nadhani kwamba sisi aote tunajua kuwa Arsenal atakuwa mmoja
wao na kupoteza alama kwao ama kuzipata dhidi yao, hiyo ni muhimu sana.”
Alisema Slot.
Kwa upande wa Arsenal waliopoteza mechi ya awali ya ligi kwa
kukubali kichapo cha mabao mawili kwa nunge dhidi ya Bournemouth, inalenga
kurejea kwa mbinu zake za ushindi Jumapili.
Kocha Mikel Arteta amewataka mashabiki kujitokeza zaidi
kushabikia timu yao ili kuwapa motisha vijana wake kupata ushindi dhidi ya
Liverpool.
“Jumapili, tunawahitaji ata zaidi, nina uhakika watajitokeza na
tutazidi kupiga hatua.“ Alisema
Arteta.
Timu ya Arsenal inakosa huduma za wachezaji Bukayo
Saka, Riccardo Calafiori na Jurrien Timber ambao wanaugusa majeraha ya misuli ya
paja, goti na misuli mtawalia.
Vile watakosa huduma za Martin Odegaard, Takehiro Tomiyasu
na Kieran Tierney ambao pia wana majeraha pamoja na William Saliba aliyepata
kadi nyekundu katika mchezo wa awali.
Liverpool nao watakosa huduma za Diogo Jota, Cornor Bradley
na Alisson Becker.
Mechi hiyo itachezwa kuanzia saa 1:30 Jumapili
usiku.