logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Uchaguzi wa FKF kwenye baadhi ya kaunti kuandaliwa tena

Hii ni baada ya wagombea wa nyadhfa muhimu kwenye uchaguzi huo kupata idadi sawa ya kura

image
na Brandon Asiema

Football15 November 2024 - 08:41

Muhtasari


  • Uchaguzi katika kaunti nyingine ikiwemo Turkana na  Homabay haukuandaliwa Alhamisi jinsi ilivyostahili kufanyika sawia na kaunti nyingine.
  • Uchaguzi wa nyadhfa muhimu katika kaunti nyingine zitarudiwa baada ya wagombea kutoshana katikamidadi ya kura walizopigiwa.

caption

Baadhi ya kaunti zitalazimika kushiriki tena uchaguzi wa kuwachagua viongozi kwenye shirikisho la soka nchini FKF, baada ya wagombea kutoshana katika kura.


Uchaguzi huo uliofanyika Alhamisi katika matawi mbali mbali kote nchini, ulishuhudia kuahrishwa kwa mchakato huyo katika baadhi ya kaunti, bodi ya uchaguzi wa FKF ikitarajiwa kuweka wazi tarehe ambazo uchaguzi huo utaandaliwa.


Aidha katika kaunti nyingine, uchaguzi utarudiwa kwa mara ya pili baada ya wagombea kutoshana kwa idadi ya kura.


Bodi ya uchaguzi wa  FKF inaoongozwa na mwenyekiti Hesbon Owilla, imesema kuwa uchaguzi katika kaunti kama vile Bungoma, Bomet, Elgeyo Marakwet, Kakamega, Embu, Narok, Samburu, Kisii, Lamu, Nandi na West Pokot kati ya nyingine zilikamilisha uchaguzi wao vyema na washindi katika nyadhfa zilizokuwa zinawaniwa kuwekwa wazi.


Uchaguzi katika kaunti za Turkana, Mandera na Homabay umeratibiwa kufanyika siku tofauti.


Vile vile, baadhi ya matawi ya FKF yatalazimika kurudia uchaguzi baada ya wagombea kupata idadi sawa ya kura kwenye nyadhfa muhimu. Kaunti za Vihiga na Nyandarua ndizo zitarejelea uchaguzi wa nyadhfa hizo muhimu.

Katika kaunti ya Nyandarua, uchaguzi wa mwenyekiti na katibu mkuu wa tawi hilo utarudiwa Jumamosi baada ya wagombea wawili Reuben Kai na Charles Thotho kupata idadi sawa ya kura huku uchaguzi wa katibu mkuu katika kaunti ya Vihiga pia ukiratibiwa kurudiwa. 

Uchaguzi za FKF kwenye ngazi ya kaunti zilihusisha mwakilishi wa wanawake kwa FKF, mwakilishi wa vijana, mweka hazina, katibu mkuu wa kaunti na mwenyekiti wa kaunti.


Wenyekiti waliochaguliwa katika kila kaunti, watashiriki katika uchaguzi wa kumchagua rais wa shirikisho katika uchaguzi utakaondaliwa Desemba 7.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved