logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Arne Slot asema mechi ya Jumapili dhidi ya Southampton ni ngumu.

Liverpool itakosa huduma za mchezaji Trent Alexander-Arnold ambaye hajarudi kushiriki mazoezi kutokana na jeraha

image
na Brandon Asiema

Football22 November 2024 - 13:07

Muhtasari


  • Kufikia sasa, Liverpool haijapoteza mechi ya ligi kuu nchini Uingereza ikiongoza msimamo wa jedwali kwa alama 28 baada ya mechi 11.
  • Virgil Van Dijk amerejea mazoezini na sasa yuko salama kucheza mechi ya Jumapili. Dijk amejiunga na wachezaji wenzake katika mazoezi ya Ijumaa ya matayarishoya mechi ya Jumapili.

caption

Kocha wa Liverpool Arne Slot amekiri kuwa mechi ya Liverpool dhidi ya Southampton siku ya Jumapili itakuwa ngumu ligi ya Uingerza inapoingia raundi ya 12.

Akizungumza katika mahojiano na wanahabari Ijumaa mchana . kocha Slot amesema kuwa timu ya Southampton ina mtindo mzuri wa kucheza licha ya kutopata ushindi katika mechi za awali.

“Southampton wamekuwa na bahati mbaya lakini mtindo wao wa kucheza ni bora, wangeweza kupata matokeo katika kila mechi. Itakuwa mechi ngumu Jumapili.” Amesema Arne Slot.

Liverpool katika mechi kumi na moja ambazo wamecheza msimu huu, wameshinda mechi tisa chini ya kocha Arne Slot na kutoka sare mechi mbili pekee.

Kufikia sasa, timu hiyo inaongoza msimamo wa jedwali laligi kuu Uingereza kwa alama ishirini na nane, alama 5 mbele ya bingwa mtetezi Manchester City.  Mpinzani wa Liverpool jumapili, Southampton yukokatika nafasi ya mwisho baada ya ushindi wa mechi moja na sare moja akiwa na alama 4.

Akizungumzia majeraha katika kikosi chake, kocha Arne amesema kuwa Virgil Van Dijk amerejea mazoezini na sasa yuko salama kucheza mechi ya Jumapili. Dijk amejiunga na wachezaji wenzake katika mazoezi ya Ijumaa ya matayarishoya mechi ya Jumapili.

Aidha, huduma za Trent Alexander-Arnold  zikakosekana kwani kwa mujibu wa kocha Arne Slot mchezaji huyo hajakuwa akishiriki mazoezi kutokana na jeraha lakini Slot amesema kuwa mchezaji huyo atarejea hivi karibuni.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved