logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Alichokisema Reece James baada ya kurejea tena uwanjani

Nahodha wa chelsea timu ya wanaume Reece James alirejea katika uwanja dhidi ya Bournemouth.

image
na Japheth Nyongesa

Football16 January 2025 - 09:52

Muhtasari


  • Tangu James kuteuliwa kuwa nahodha wa chelsea, ameanizishwa tu kwenye michezo nane yenye michuano mikali.
  • James aliifungia Chelsea bao lililowafanya kupata alama moja dhidi ya wahasimu wao Bornemouth, alifunga kupitia free kick.


“Sijakua na tamaa ya kutokuwepo kwa muda mrefu”

Nahodha wa chelsea timu ya wanaume Reece James amerejea katika uwanja akicheza kwenye ligi kuu ya Uingereza .

James aliifungia chelsea bao lililowafanya kupata alama moja dhidi ya wahasimu wao Bournemouth, alifunga kupitia free kick.

Kufikia sasa nahodha huyo amekosa mechi 21 katika mashindano yote kutokana na jeraha la misuli ya paja akifaulu kucheza mechi  5 tu pekee za ligi kuu uingereza msimu huu.

Alionekana mwenye furaha zaidi  baada kupiga free kick hiyo na kufunga huku meneja wa timu ya taifa Uingereza Thomas Tuchel akimutizama.

“Ulikuwa wa upweke na kuudhi”. James alliambia shirika la habari la BBC kuhusu muda wake Akiwa inje.

“ Nina furaha sana kurejea uwanjani na kusaidia timu yangu”

“Matumaini ni kuwa sawa mpaka mwisho wa msimu,”

James amekuwa inje kwa muda kutokana na majera ya goti na harmstring kwenye misimu kadhaa iliyopita.

Tangu James kuteuliwa kuwa nahodha wa chelsea, ameanizishwa tu kwenye michezo nane yenye michuano mikali.

Mara ya mwisho kuonekana alicheza dakika nane tu pekee dhidi ya Arsenal  mwezi novemba huku akifunga bao lake la mwisho  mwezi Oktoba 2022 dhidi ya AC Milan.

James mwenye uraia wa Uingereza alirejea uwanjani Jumapili baada ya kukaa nje kwa muda wa miezi miwili akicheza dhidi ya Morecambe kipindi cha kwanza pekee kwenye michuano ya kombe la FA.

James ambaye ameishindia timu yake ya taifa vikombe 16 aliulizwa kuhusu uwezekano wake wa kurejea kuichezea timu ya taifa na hili ndilo alilosema, “ Kwa sasa mkufunzi ni Thomas Tuchel  na anaelewa uwezo wangu,”

James alikuwa na nafasi nzuri wakati Thomas Tuchel akiwa mkufunzi wa timu ya chelsea  mwaka 2021 akiwa kwenye kikosi klichoishindia chelsea  kombe la mabingwa ulaya huko German.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved