logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Maresca azungumzia wachezaji wa Chelsea ambao Hawatakuwepo dhidi ya Brighton Jumamosi

Walinzi Wesley Fofana na Benoit Badiashile wamekosekana kwa muda mrefu.

image
na Japheth Nyongesa

Football07 February 2025 - 14:22

Muhtasari


  • Chelsea watakua wakicheza Kesho na Brighton & Hove Albion mwendo wa saa tano usiku kwenye kombe la FA mzunguko wa nne. 
  • Mara ya mwisho mahaasimu hawa wawili kukutana huko Stamford Bridge , mchuano ulikamilika 4-2 kwa faida ya Chelsea.


Kocha mkuu wa Chelsea Enzo Maresca akihutubia wanahabari ameweka wazi wachezaji ambao hawatakuwepo kutokana na majeraha.

Nicolas Jackson maamuzi ya kushiriki katika mchezo huo wa kesho Bado hayaamuliwa kutokana na jeraha alilopata usiku wa Jumatatu walipokuwa wakicheza dhidi ya West Ham United.

Jackson aliondolewa inje mwanzoni mwa kipindi cha pili baada ya kupata jeraha la Hamstring. Mark Guiu ambaye aliingia nafasi ya Jackson pia hatakuwepo kutokana na jeraha alilopata mwishoni mwa mchuano.

"Marc ana jeraha baya kwa hivyo hatakuwepo. Huenda akawa nje kwa muda mrefu, tunangoja kujua muda kiasi gani labda wiki kadha. Nicolas anaeza kuwa sawa kabla ya mechi lakini kumuchezesha ni kuhatarisha, tutaona wakati huo, maumivu yake si makubwa. alieleza.

Walinzi Wesley Fofana na Benoit Badiashile wamekosekana kwa muda mrefu.

Enzo pia amethibithisha kutokuwepo kwa kiungo wa kati Romeo Lavia ambaye alikutana na majeraha yake wakati wa mechi yao dhidi ya Bournmouth mwezi jana.

"Romeo bado yupo kwenye harakati za kurudi ila bado ana mwendo mrefu mbele yake, alieleza Mkufunzi wa Chelsea Enzo.

Chelsea watakua wakicheza Kesho na Brighton & Hove Albion mwendo wa saa tano usiku kwenye kombe la FA mzunguko wa nne. 

Brighton watakuwa wenyeji wa mchuano. mara ya mwisho mahaasimu hawa wawili kukutana huko Stamford Bridge , mchuano ulikamilika 4-2 kwa faida ya Chelsea.

Cole Palmer akifanikiwa kufungia Chelsea mabao yote manne huku Quomah Maleba na G. Rutter akizawazisha kwa upande wa timu ya Brighton.

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved